Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jul 25, 2015

WANASIASA CHADEMA, CCM NA ACT KUTOANA JASHO NAFASI ZA UBUNGE KIGOMA



WAKATI Watanzania wakisubilia kupiga kura ya kuwachagua viongozi watakao waongoza katika uchaguzi Mkuu utakaofanyia mweze Octoba mwaka huu, Wanasiasa mbalimbali mkoani Kigoma wamejitokea kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya  kuviwakilisha vyama vyao katika nafasi ya Ubunge.

Mkoa wa Kigoma wenye Wilaya  sita  ambazo ni pamoja na Wilaya ya Kigoma, Kasulu, Kibondo, Uvinza, Kakonko na Buhingwe, katika uchaguzi wa mwaka huu umegawanywa katika majimbo nane ya uchaguzi ambayo ni Kigoma Mjini, Kigoma Kaskazini, Kigoma Kusini, Kasulu Mjini, Kasulu Vijijini, Buyungu, Muhambwe (Kibondo) na Manyovu (Buhigwe). 


Aidha tayari wanasiasa kupitia vyama hasimu hapa nchini Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walishachukua fomu na kurudisha ili kupata ridhaa ya vyama vyao katika kinyanganyiro cha nafasi ya Ubunge.

Katika Jimbo la Kigoma mjini, waliojitokeza kuchukua fomu na kurudisha kupitia CHADEMA ni pamoja na Mwanasheria Daniel Rumenyela, Kabwar Shaban, Ally Mleh na Francis Mangu. Wakati CCM wakiwa ni Mwenyekiti wa chama hicho Mkoani hapa, Dk. Waridi Amani Kaboulou, Elisha Zilikana, Gabriel Sospeter na Zuberi Madie.


Wakati vyama hivyo pinzani vikiandaa wagombe ambao watapambana katika uchaguzi ujao katika Jimbo hilo, Zitto Kabwe ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kupita CHADEMA kabla ya kufukuzwa, alichukua  fomu ya Ubunge ili kugombea katika Jimbo la Kigoma mjini kupitia chama kipya cha  ACT.

Katika Jimbo la Kigoma Kaskazini, waliojitokeza kuchukua fomu na kurudisha kupitia CHADEMA  ni pamoja na Mjumbe wa Kuchaguliwa Kamati kuu Taifa wa Chama hicho, Dk Yared Fubusa, Kamsige Fabian, Munisi Faraja na  Akrani John.


Wakati CCM wakiwa ni Peter Serukamba aliyekuwa akiliwakilisha Jimbo la Kigoma Mjini, Halimeshi Kahena Manyonga, Juma Athumani Matete, Robison Fulgence Lembo, Mahwago Kayandabila, Hamisi Betese, Omari Mussa Nkwarulo, Dk. Ernest Rugiga na Robert Yohana.

Jimbo la Kigoma Kusini, waliochukua fomu na kurudisha kupitia CHADEMA) ni mtu mmoja tu ambaye ni Bonyimana Michael. Wakati CCM wakiwa ni Nashoni Bidyanguze, Waziri Mourice, Thomas M. Sengai, Gulamhussein Kiffu Shabani, Salum I. Sasilo, Iddi Ndabona, Dr. Norbert N. Shemetse, Hasna Mwilima, Dr. Ernest Nsumila, Ally Ayubu Kalufya, Manju Salumu Msambya, January Kizito, Dismas Clemence Malele, Jumanne M. Hussein na Majaliwa Zuberi.
Kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe kulia akimtambulisha Mbunge wa Kasulu Mjini aliyemaliza muda wake Moses Machali ambaye amejiunga rasmi na ACT-Wazalendo

Katika Jimbo la Manyovu (Buhigwe), waliojitokeza kuchukua fomu na kurudisha kupitia CHADEMA ni pamoja na Baslius Budida, James Japhet, Dk. Henry Wilsom na Balakuba Ndoloma huku waliochukua kupitia CCM ni Albert Obama, Abia Mnyabari, Phillipo na Kavejuru Eliadoli.

Katika Jimbo la Muhambwe (Kibondo), waliojitokeza kuchukua fomu na kurudisha kupitia CHADEMA ni mtu mmoja  ambaye ni Nick Kilunga, wakati CCM wakiwa ni Eng. Atashiste Ndikije, Moshi Nyakamwe, Emmanuel Gwegenyeze, Dk Joseph Tutuba, Jarud Tumaini, Dk. Witonze Erick, Edger Mkosamali, Regina Kayabu, Dk. Richard Kijarabs, Mapigano Nduhirubusa, Anderson Njiginya.

Jimbo la Buyungu, waliojitokeza kuchukua fomu na kurudisha kupitia CHADEMA ni pamoja na Kasuki Samson, Jiles Rungwana, Olafu Kaboboye, Gaston Garubinand, Rose Ntirulasanye, Ashura Mashaka. CCM  ni Eng. Christopher Chiza, Carlos Gwamagobe, Ernest Basaya, Liberi Ndabita, Modest Apolinary na  Nsakila Kabende

Sambamba na hayo, Moses Machali aliyekuwa Mbunge wa Kasulu Mjini kupitia NCCR Mageuzi baada ya kukihama chama hicho na kujiunga na ACT, alichukua fomu ili kukiwakilisha chama hicho katika jimbo hilohilo huku akiungana na Mrisho Mzingwa, Askofu David Mpango na  Hamza Mtunu.