Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Nov 16, 2015

ACT YAENDELEZA UBABE VITI VYA UDIWANI KIGOMA

BAADA ya Uchaguzi wa Kiti cha Udiwani kata ya Kagera katika Manispaa ya Kigoma-Ujiji kuahirishwa kutokana na picha ya mgombea wa ACT-Wazarendo kukosekana kwenye urodha ya wagombea, uchaguzi huo umefanyika jana na kumalizika kwa amani huku ACT ikiendelea kujiongezea viti vya udiwani.


Baada ya uchaguzi na uhesabuji wa kura kumalizika, Mismamizi Mkuu wa uchaguzi katika kata hiyo Stanslaus Ntatiye, ametangaza matokeo ambapo  mgombea  Ismail Mahmud Hussein ACT alipata kura  959, Keberezo Gregory Fednand  CCM 9 kura 18, Damas Rashid CHADEMA kura 497, Mary Jeremiah – Jahazi Asilia kura 8.

Kwa mujibu wa idadi hiyo ya kura, Msimamizi Ntatiye, amemtangaza Ismail Mahmud Hussein wa ACT kuwa Diwani mpya wa kata ya Kagera huku akiungana na madiwani wengine 18 waliochaguliwa Octoba 25.

Ushindi huo wa ACT-Wazarendo umewafanya kuongeza viti vya udiwani na kuongoza katika manispaa hii kwa kuwa na viti 13 wakati CCM ikiwa na viti vitano na CHADEMA kiti kimoja tu.