Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Nov 17, 2015

MAGABA SECONDARY KUTOA ELIMU BURE KWA WANAFUNZI



UONGOZI wa shule ya secondary Magaba iliyoko katika kijiji cha Nyakitonto Wilaya ya  Kasulu mkoani Kigoma umeadhimia kutoa elimu bure kwa watoto wanaotoka katika familia maskini pamoja na wenye ulemavu wa viungo.
Wanafunzi waliohitimu kidato cha nne katika shule ya Secondary Magaba wakiwa kwenye mahafari ya yao na ya pili kwa shule hiyo.
Hayo yalibainishwa  hapo jana na Mkurugenzi na mmiliki wa shule hiyo Leonard Magaba wakati  akizungumza na wazazi, walezi, wanafunzi wa shule hiyo pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali ya wilaya ya Kasulu katika mahafari ya pili yaliyofanyika shuleni hapo.

Magaba alisema kuwa , kutokana na kutambua kuwa jamii ya kitanzania bado inakabiliwa na umasikini wa kipato sambamba na baadhi ya watoto kushindwa kusoma kwasababu ya ulemavu, shule hiyo itawagharimia  watoto hao ili nao wapate haki yao ya kuelimika.
Wanafunzi waliohitimu kidato cha nne katika shule ya Secondary Magaba wakiwa kwenye mahafari ya yao na ya pili kwa shule hiyo.
Aidha  Magaba alisema kuwa, kitendo cha kusomesha watoto bure anakichukulia kama kutimiza ahadi yake ambapo  kutokana na yeye kuzaliwa katika familia masikini isiyokuwa na elimu alishindwa kuendelea na masomo ya sekondari baada ya kuhitimu darasa la saba na  aliweka malengo ya kujenga shule ya sekondari na iwapo atafanikiwa atawasaidia watoto wapate elimu na kuisaidia jamii yake.

“Sikufanikiwa kusoma hadi elimu ya juu japo nilikuwa napenda kusoma kutokana na wazazi wangu kuwa na uwezo mdogo kifedha lakini hata hivyo ninamshukuru Mungu kuwa hivi nilivyo,  malengo ya kujenga shule ili niwasaidie ndugu zangu yametimia na sasa nimekuwa na mchango kwa kuisaidia jamii yangu’’ Alisema Bw. Magaba
Mkurugenzi na mmiliki wa shule ya secondary Magaba Leonard Magaba wa tatu kutoka kushoto akiwa na viongozi wa serikali katika mahafari ya kumali kidato cha nne katika shule yake.


Alisema kuwa, kuanzia mwakani 2016 shule yake imeweka utaratibu wa kuchukua mwanafunzi mmoja kutoka kila shule ya msingi ndani ya kata hiyo ya Nyakitonto na kumsomesha bure kwenye shule yake hadi kidato cha nne ila walengwa ni wanafunzi waliofauru huku wakiwa ni yatima wasiokuwa na uwezo kifedha, walemavu ama watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

“Mpaka sasa natambua kwamba kuna watoto waliopo shule za misingi na wanafauru mitihani yao ya kwenda sekondari lakini wanaoshindwa kuendelea na masomo kutokana na umasikini uliokithiri, sasa ili kuisaidia serikali kuhsu suala la elimu watoto hao nitawapatia elimu ili nao wajitengenezee maisha ya baadae’’ alisema Magaba.


Magaba aliongeza kuwa,  kadri Mungu atakavyomjalia ataongeza utaratibu huo na kuchukua wanafunzi katika ngazi ya tarafa, Wilaya na hadi mkoa ili kuwasomesha pia amewataka wanajamii kushiriki kwa kuwachangia watoto na jamaa zao kuwasomesha ili kupigana na adui ujinga.

Kwa upande wao wazazi na wadau mbali katika sekta ya elimu walifurahishwa na kauli hiyo na kuzitaka shule zingine binafsi kuiga mfano huo kwani utasaidia kuwakomboa watoto walio katika mazingira hayo ambao wamekuwa wakishindwa kupata elimu kutokana na ugumu wa maisha.

Obadia Mbonye ambaye ni mmoja wa wazazi hao  alisema kuwa maamuzi hayo ni ya kuigwa na kwamba yatasaidia kuokoa watoto ambao wamekosa fursa ya kuendelea na elimu ya sekondari kutokana na kuwa masikini wa kipato ama walemavu huku wakiwa na uwezo wa kitaaluma.
Wanafunzi waliohitimu kidato cha nne katika shule ya Secondary Magaba wakiwa kwenye mahafari ya yao na ya pili kwa shule hiyo.
Nae Mgeni rasmi katika mahafari hayo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu vijijini  Joseph Ngoswe alipongeza mpango huo wa kusomesha watoto wasiojiweza na alizitaka shule zingine za binafsi wilayani humo kuiga mfano huo kwani kila mzazi anastahiri kumjari mtoto wa mwenzake

“Mtoto ukimlea katika njia impasayo kamwe hataiacha hadi akiwa mzee na Tanzania inahitaji vijana waliosoma na sio wanaoshinda vijiweni kwa kukosa ajira, kitendo cha kuwasomesha watoto wasiojiweza ni cha kuigwa na jamii nzima kwa lengo la kuinua elimu hapa nchini” alisema Ngoswe.