Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 24, 2016

LIVERPOOL YASHINDA, MAN UTD NA KOCHA WAKE WAZOMEWA


Klabu ya Manchester Unitrd imejikuta ikipoteza mchezo wake wa ligi baada ya kuambulia kipigo cha bao moja kutoka kwa Southampton katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa Old Traford.

Bao pekee la Southampton lilifungwa na mchezaji mpya wa timu hiyo Charlie Austin ikiwa ni dakika saba baada ya kuingia akitokea benchi..

Manchester United walishindwa kufanya mashambulizi yoyote ndani ya dakika 90 za mchezo kitu kilichofanya mashabiki wa timu hiyo kuanza kuwazomea wachezaji na kocha wao Louis Van Gaal.

Kwa upande wa Liverpool wao walipata ushindi wa mabao 5-4 dhidi ya Norwich City na kuifanya timu hiyo kupanda hadi nafasi ya saba ya msimamo wa ligi.

Robert Firmino aliiweka kifua mbele Liverpool baada ya kufunga bao dakika ya 18 ya mchezo lakini Dieumerci Mbokani alisawazisha kwa upande wa Norwich kabla ya bao La Steve Naismith kuiweka mbele Norwich kwa mabao 2-1.

Wes Hoolan alifunga bao la tatu kwa penalti hivyo Norwich kuwa mbele kwa mabao 3-1 lakini baadae Jordan Henderson alifunga bao la pili kwa Liverpool na Frimino akaongeza bao la tatu na mchezo kuwa 3-3.

James Milner alifunga tena kwa upande wa  Liverpool lakini baada ya muda Sabastian Basson akisawazisha na mabao yakawa 4-4 ila zikiwa zimesalia dakika 2 mpira kuisha Adam Lallana akafunga bao la Ushindi hivyo Liverpool kuondoka na ushindi wa mabao 5-4.

Matokeo mengine ni kama ifuatavyo.
Norwich 4 - 5 Liverpool 
Crystal Palace 1 - 3 Tottenham 
Leicester 3 - 0 Stoke 
Man Utd 0 - 1 Southampton 
Sunderland 1 - 1 Bournemouth 
Watford 2 - 1 Newcastle  

West Brom 0 - 0 Aston Villa 
West Ham 2 - 2 Man City