Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 25, 2016

MVUA YALETA MADHARA KIGOMA



Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya mkoa Kigoma zimeleta athari kwa kuharibu miundomibinu ya madaraja katika mfereji wa Lubengera uliopo Manispaa ya Kigoma Ujiji unaotumika kupitisha maji machafu kwenda ziwa Tanganyika.
Daraja la kwa Jaffar lililopo eneo la soko kuu mjini Kigoma likiwa limebomoka na kulazimika barabara ya Kaya inayopita darajani hapo kufungwa kufuatia mvua kubwa zilizonyesha usiku wa kuamkia jana na kuathiri madaraja mbalimbali ya Mfereji wa Lubengera ambao hutumika kupitisha sehemu kubwa ya maji taka ya mji huo yanayoingia ziwa Tanganyika.
Kufuatia kubomoka kwa madaraja hayo na serikali kulazimika kuifunga barabara ya Kaya Road ambayo daraja la kwa Jaffar limaethiriwa na mvua hiyo wananchi wamelalamikia viwango duni vya ujenzi wa madaraja hayo uliofanywa na makandarasi wazawa na hivyo kuitia hasara serikali.


Wakizungumza kuhusiana na hali hiyo Mussa Abbasi na Ayubu Mlagile wamesema kuwa badala ya serikali kuendelea kupoteza mamilioni ya shilingi kuwapa wakandarasi wazawa miradi hiyo ya ujenzi wa madaraja na kuharibika baada ya vipindi vifupi wametaka kazi hiyo wapewe wakandarasi wa makampuni ya kichina kutokana na utaalam walionao na vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi.


Akizungumzia kubomoka kwa madaraja hayo Diwani wa kata ya Kigoma Mjini,Hussein Kalyango amesema kuwa tayari viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Mkuu wa mkoa Kigoma, Issa Machinya wametembelea kuona uharibifu huo na kwamba Hamashauri itachukua hatua za haraka kukabiliana na uharibifu huo.