Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Feb 19, 2016

BIMA YA AFYA YATOA HUDUMA ZA VIPIMO BURE KWA WAKAZI WA MKOA HUO


Afisa Masoko wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Kigoma, Evance Ndyamukama.

Mfuko wa hifadhi ya Taifa wa bima ya afya (NHIF) mkoa wa Kigoma umeanzisha huduma ya upimaji wa afya za kwa wakazi wa kigoma lengo ikiwa ni  kuwarahisishia huduma ya vipimo wakazi hao pamoja na kutoa hamasa kwa wananchi kujiunga na mfuko huo.

Akizungumzia zoezi hilo meneja wa mfuko wa huo Mkoa wa Kigoma Elias Odhiambo alisema, zoezi hilo lilianza jana mkoani hapo ambapo lengo kuu ni kurahisha upimaji afya kwa wakazi hao sambamba na kutoa elimu kwa wakazi hao kujiunga na mfuko wa Bima ya afya.

“tunatoa huduma ya vipimo bure ambapo tumewatangazia wananchi iliwaweze kufika viwanja vya community centre mwanga mjini Kigoma lengo letu ni wakazi wote kupata huduma hyo lakini pia tunawahamisha kujiunga na mfuko wa bima ya afya ili kuona umuhimu wa malipo kabla” alisema Odhiambo.

Aidha alisema zoezi hilo litafanyika kwa muda wa siku tano kuanzia jumatatu hadi ijumaa ambapo alisema vipimo vinavyotolewa ni urefu na uzito, sukari, presha macho pamoja na huduma ya vipimo vya virusi vya ukimwi HIV ambayo inetolewa kwa kushirikana na kitengo cha CTC cha hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Kigoma Maweni.