Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Mar 5, 2016

CCM KIGOMA YAWAFUKUZA VIONGOZI NA WANACHAMA WAKE

VIONGOZI na wanachama 25 wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kigoma wamefukuzwa uanachama wa chama hicho kutokana na usaliti uliofanyika ndani ya chama wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika oktaba 25, 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa CCM Mkoa  Katibu wa CCM chama hicho mkoa wa Kigoma Naomi Kapambala alisema, uamuzi huo umetolewa katika kikao cha halmashauri kuu cha Mkoa kilichofanyika march 2016 kilicholenga kufanya tathimini ya uchaguzi huo.

Naomi alisema kuwa baaada ya uchaguzi mkuu kufanyika chama kilianza kufanya tathimini lengo ikiwa ni kubaini mafanikio pamoja na changamoto zilizojitokeza katika chama hicho ili kujua nini kifanyike kuepuka changamoto zilizojitokeza kipindi hcha uchaguzi huo.

Alieleza kuwa sababu mbali mbali zilizochangia wanachama hao kuvuliwa uanachama ni kuhama chama kutokana na sababu ya kutoteuliwa kuwa wagombea wa nyadhifa mbalimbali katika uchaguzi huo na viongozi waliosaliti chama kwa kutumia nguvu ya ushawishi wa kukiangusha chama hicho pamoja na kugombe kupitia vyama pinzani baada ya kukosa nafasi CCM.

''tulifanya tathimini na kugundua kuwa baadhi ya wanachama ambao walikuwa siyo waaminifu kipindi cha uchaguzi mkuu walikuwa wakikisaliti chama, hata viongozi waliogombea ubunge na kushindwa kwenye  kura za maoni tumewavua uanachama ili watupishe sisi tuendelee kutekeleza ilani ya chama''alisema Kapambala.
Aidha wanachama waliofukuzwa ni Venance Mpologomi, Paul bahinda, Damasi Shetei,Gidioni Bunyanga, Edger Mkosamali, Pili Waziri, Pendo Jumanne, Robinson Lembo, Juma matete, Idd Lugundanya, Juma Kifuku, Edga Bisoma, Staphord Kumuhanda, Jenoveva Bisana, Salehe Anatori, Abdallah Chugu, Atanas Andrea, Bigilimana Vyanda, Jonas Kafyiri, Isack Braytony, Christopher Chiza, Fanuel Kasogota, Laulent Bikulamuchi, Ibramu Shikuzilya na Paul Chabandi.
 
Akizungumzia zoezi hilo Katibu wa jumui ya ya wazazi Mkoa wa Kigoma Staney Mkandawile alisema,  kwa sasa hivi kazi iliyopo ni kutekeleza ilani ya chama na kuumunga mkono  Rais John Magufuli kauli mbiu ya hapa kazi tu ili kuweza kutekeleza majukumu  ya Chama.

Mkandawile alisema kuwa Chama hakitamuonea aibu mwanachama yeyote na kwamba bora chama kibaki na wanachama wachache ndani ya chama ambao wapo tayari kufanya kazi za chama na kukipenda kwa dhati lengo ikiwa ni kutekeleza  ilani ya chama hicho.