Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jul 4, 2015

WAKIMBIZI WAATHIRI HUDUMA ZA AFYA KIGOMA



MKOA wa Kigoma umekumbwa na adha ya upungufu mkubwa wa vifaa tiba katika vituo vyake vya afya, zahanati na hospitali, hali inayotishia usalama wa wananchi.

Aidha hiyo inatokana na kuwepo kwa wimbi kubwa la raia kutoka nchini Burundi wanaoingia mkoani hapa kutafuta hifadhi, kufuatia machafuko ya kisiasa yanayoendelea katika nchi hiyo jirani.
Hayo yalielezwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Dk. Leonard Subi alipokuwa akipokea msaada wa vifaa tiba, vilivyotolewa na Shirika la Actionaid, katika hafla iliyofanyika juzi.
Baadhi ya vifaa tiba na magodoro yakishushwa katika hospitali ya mkoa mwa Kigoma Maweni baada ya kukabidhiwa.

Alisema kuwa hivi sasa vituo vingi vya kutoa huduma za afya mkoani Kigoma vinakabiliwa na tatizo hilo la upungufu wa vifaa tiba, huku kukiwa na changamoto nyingine ya magonjwa ya kuhara na kipindupindu ambapo watu 38 walisharipotiwa kufariki dunia.

“Baada ya magonjwa ya mlipuko kutokea kutokana na hari ya uchafu iliyosabishwa na kutokuwepo kwa huduma za kijamii zenye kukidhi wingi wa watu, Serikali ya mkoa kwa kushirikiana na  idara ya afya mkoani hapa tulijitahidi kutoa huduma kwa wagonjwa ambao wengi wao walikuwa wakimbizi.

“Kufuatia hali hiyo, vifaa tiba vilivyokuwa vikitumika ni vile vilivyowekwa kwa ajiri ya Watanzania kabla ya mashirika mengine kuanza kutoa msaada wa vifaa hivyo,” alisema Mganga Mkuu huyo wa Mkoa wa Kigoma.
Mkuu wa mkoa wa Kigoma Issa Machibya katikati akipokea baadhi ya vifaa tiba kutoka kwa Dk. Azaveli Lwaitama ambaye ni Muhadhiri Mwandamizi na Mwenyekiti Msaidizi wa  wa Shirika la Actionaid Tanzania.

Dk. Subi alisema hadi sasa kuna wakimbizi wapao 100,025 walioko kambi ya Nyarugusu, ambapo Vijiji vya  Mwakizega, Ilagara, Kalago Wilaya ya Uvinza, Kaseke na Manispaa ya Kigoma kuna wagonjwa wa kipindupindu walioripotiwa kufikia idadi ya watu wanane. 

Kwa upande wake Mkuu wa Programu na Sera wa Shirika la Action Aid, Josephat Mshigati alisema kwenye hafla hiyo kuwa, shirika hilo limetoa dawa, vitendanishi, magodoro, groves (medicines and medical supplies/ equipment) kwa Serikali ya mkoa wa Kigoma.
Baadhi ya vifaa tiba na magodoro yakishushwa katika hospitali ya mkoa wa  Kigoma Maweni baada ya kukabidhiwa.

“Vifaa hivi vimegharimu kiasi cha sh. 65,425,000 ambapo ukijumlisha na usafiri wake inakuwa sh. 73,425,000. Lakini pia tumefanya hivi ili kuyakumbusha mashirika mengine kuungana na sisi kutoa msaada wa vifaa tiba ili kumaliza kabisa tatizo hili,” alisema Mshigati.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Dk. Leonard Subi akizungumza wakati wa kukabidhiwa vifaa tiba.
Baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Kigoma akiwemo Ashura Japhari na John Jeremiah walisema hivi sasa watu wengi mkoani hapa wanapata tabu kupata dawa punde wanapokwenda kupima maladhi.
Josaphat Mshigati ambaye ni Mkuu wa Programu na Sera wa Action Aid, akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa tiba.