Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Nov 24, 2015

AKINA MAMA WAWAJIA JUU VIONGOZI WA MASANGA GROUP KUHUSU UBADILIFU NDANI YA KIKUNDI



WANACHAMA wa Kikundi cha Hisa cha kina Mama, Masanga Group, kilichoko mtaa wa Masanga katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, wameingia katika mgogoro na viongozi wa kikundi hicho kufuatia kutopewa pesa zao ambazo walikuwa wakiweka kama hisa na kuwatuhumu viongozi hao kwa ubadhirifu.

Wakizungumza na Blog hii, kina mama hao wamedai kuwa walipaswa kuvunja hisa na kila mwanachama kupatiwa mtaji aliowekeza pamoja na faida kwa mujibu wa taratibu tangu mwezi Agosti mwaka huu, lakini hadi sasa viongozi wao wamekuwa wakiwapa majibu yasiyoridhisha kuhusu pesa zao.
Baadhi ya akina mama mkoani Kigoma (Picha haihusiani na Habari)
Katika ofisi ya Polisi Jamii kituo cha Masanga ambapo akina mama hao walikusanyika kwa ajili ya kutafuta suluhu ya suala hilo chini ya mwenyekiti wa mtaa, baadhi ya wanachama hao wakiwemo Dainesi Damian na Mariam Kasunzu , wamepinga kauli ya viongozi wao kuwa pesa hizo ziko mikononi mwa baadhi ya wanachama waliokopa.

“Madeni yalioko nje ni kama shilingi million 12 hadi 16 na mitaji ya watu walioweka pesa zao ni zaidi ya Milioni 38, sasa hapo tunashindwa kuelewa ni kwanini watu wanashindwa kugawiwa pesa zao nawakati pesa zipo tena zaidi ya milioni 38” amehoji Mariam Kasunzu.

Aidha wanachama hao wamewatuhumu viongozi wao kwa kukiuka taratibu za uendeshaji wa kikundi hicho kutokana viongozi kutowapa mikopo wanachama wanaotaka kwa njia harari bali hutoa mikopo kinyume na taratibu.

“Kawaida sisi tunakopa mkopo kwa liba ya asilimia 10 lakini ukiomba mkopo wa asilimia 10 kwenye kitabu unaambiwa hakuna pesa hata kama umeomba shilingi 50,000/=, lakini ukiomba mkopo wa pembeni wa liba ya asilimia 20 ambazo katibu aliamua kuwakopesha wanawake wenzake kwa maslahi yake unapewa hata laki tano” amesema Damian

Kwa upande wake Katibu wa Kikundi hicho cha Hisa, Alijumo Seme, alikanusha tuhuma za ubadhirifu zilizoelekezwa kwao ambapo alisema hatua zimeanza kuchukuliwa kwa wanachama wenye madeni na tayari taratibu za kuwafikisha Polisi zinafanyika.

Nae Mwenyekiti wa kikundi hicho, Salma Sabuhoro, amekiri ukiukwaji wa baadhi ya taratibu za uendeshaji wa kikundi likiwemo suala la mikopo kitu kilichosababisha wanachama kutoelewana na viongozi.