Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Nov 23, 2015

RAIA WA KIGENI WAISHIO KIGOMA WATAKIWA KUTOKUPUUZA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI WAO BAADA YA KUKWAMA



BAADA ya zoezi la uandikishaji wa Raia wa kigeni nchini kukwama, Uhamia Mkoa wa Kigoma imewataka raia hao kutokupuuza zoezi hilo kwani litaendelea baada ya kutatua chamngamoto zilizojitokeza awali.

Uhamiaji mkoani hapa ilikuwa ikifanya zoezi hilo  kwa kushirikiana na  Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) ambao ndio wadhamini, huku kukuwa na lengo kwa serikali kuwatambua wageni waishio nchini sambamba na kuwapa uraia wageni watakaokuwa tayari pia kwa wale watakaohitaji kurudi nchini kwao kurudishwa na IOM.
Mmoja wa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na familia yake wakiwa wameshika CARD walizopewa baada ya kuandikishwa katika hatua ya kwanza ya zoezi hilo
Akizungumza na Blog hii Ofisini kwake, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kigoma Naibu Kamishina  Maurice Kitinusa, alisema kuwa, zoezi la uandikishaji wa raia walowezi lilitakiwa kufanyika katika wilaya zote za mkoa huu lakini kutokana na changamoto zilizokuwa nje ya uwezo zoezi hilo lilikwama katika hatua ya kwanza tu.

Alisema kuwa, zoezi hilo lina hatua tatu ambapo lilikwama katika hatua ya kwanza na hatua hiyo ilikamilika katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, Kigoma vijini na baadhi ya vijiji katika wilaya ya Uvinza kwahiyo wilaya za Kasulu na Kibondo zoezi hilo lilikuwa bado halijaanza.
Afisa uhamiaji mkoani Kigoma akiendelea na zoezi la uandikishaji wa Raia walowezi katika hatua ya kwanza ya zoezi hilo kabla ya kusitishwa
“Kwahiyo tumeshindwa kuendelea na hatua zinazofuata kwasababu hata hatua ya kwanza bado haijakamilika na kwa wilaya zingine haijaanza kabisa endapo tungekuwa tumeshakamilisha hatua ya kwanza sasahivi tungekuwa tupo kwenye hatua ya pili au ya tatu” alisema Kitinusa

Aidha Kitinusa aliwataka raia wote walowezi kuwa na  subira mana zoezi hilo litaendelea kwa hatua zilizobaki na kwa wilaya ambazo lilikuwa halijaanza litaanza ili kufikia malengo na muda wa kuanza upya  matangazo yatatolewa ili raia wote wawe na taarifa.

Akizungumzia Changamoto zilizosababisha zoezi hilo kukwamba Kitinusa alisema kuwa, kukosekana kwa Pesa za kutosha, uchache wa Maafisa uhamiaji na vitendea kazi kama magari ndio kulisbabisha zoezi kukwama.

 
“Mkoa ni mkubwa na kuna viijiji ambavyo havifikiki kirahisi hivyo magari yanatakiwa ya kutosha pia ni lazima kuwepo na maafisa uhamiaji wakutosha ili kuwatawanya maeneo yote” alisema Kitinusa.

Kitinusa aliongeza kuwa, kwasasa wanasubiri serikali ikae na wafadhiri wa zoezi hili ambao ni IOM ili kupanga kuanza upya zoezi hilo na kushughurikia changamoto zilizosababisha zoezi la awali kukwama ili zoezi likianza lisikwame tena.

Hata hivyo Kitinusa, aliwataka raia walowezi ambao wameshakamilisha zoezi katika hatua ya kwanza watunze kadi walizopewa na maafisa uhamiaji ili zoezi likianza upya iwe rahisi kwao kuendelea na hatua zinazofuata pia baada ya kukamilika kwa zoezi raia wote ambao walipuuzia zoezi hilo hawatoruhusiwa kuendelea kuishi nchini.

"Kadi zile ni za muhimu sana pia inamfanya mtu aendelee kuishi nchini kwa kutumia hizo kadi wakati akisubiri hatua zingine zilizobaki katika zoezi zima" alisema Kitinusa.
CARD zilizokuwa zikitolewa na Uhamiaji baada ya kuandikishwa katika hatua ya kwanza ya zoezi hilo
Awali wakizungumzia kukwama kwa zoezi hilo raia wa walowezi mkoani hapa, walisema kuwa wakati zoezi hilo linaanza liliwapa matumaini ya kuishi nchini kwa amani na wengine kurudi katika nchi zao ila baada ya kukwama wanashindwa kuelewa nini hatima yao.

John Bigilimana kuoka nchini Burundi alisema kuwa baada ya kuambiwa maelengo ya zoezi hilo aliamua baada ya kukamilika arudishwe nchini kwao ili akaanze maisha mapya katika nchi yake badara ya kukaa ugenini ila baada ya kukwama haelewi nini kitakachofuata baadae

Asajile Hamisi ambaye ni raia wa Congo alisema kuwa, suala linalowachanganya ni zoezi kukwama bila kuambiwa ni kama litaendelea au la na akaomba serikali iwafahamishe kama zoezi lipo au halipo ili wajue kuliko kusubiri kitu ambacho kakipo.
Baadhi ya raia kutoka nchi za ukanda wa maziwa makuu waliokuwa wakiishi bila vibali mkoani Kigoma waliokuwa  wamejitokeza kuandikishwa katika zoezi la uandikishaji hatua ya kwanza kabla ya kukwama.
“Mimi kwa upande wangu niko na ndungu zangu watatu na wote tumeshakamilisha hatua ya kwanza  na vyetu tulivyopewa tunavyompaka sasa pia maazimiao yetu ni kuwa raia wa Tanzania mara baada ya zoezi kukamilika mana shughuri zetu zote tunazifanyia huku hatuoni haja ya kurudi Congo tukawe maskini, hivyo tunaomba serikali itwambie kama tuendelee kusubiri au la” alisema Asajile.
Baadhi ya raia kutoka nchi za ukanda wa maziwa makuu waliokuwa wakiishi bila vibali mkoani Kigoma waliokuwa  wamejitokeza kuandikishwa katika zoezi la uandikishaji hatua ya kwanza kabla ya kukwama