Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Nov 27, 2015

KESI YA KAFULILA YAPIGWA KALENDA



BAADA ya aliyekuwa mgombea ubunge katika jimbo la Kigoma Kusini, David Kafulila kufungua kesi ya kupinga matokeo yaliyompa ushindi mgombea wa CCM Hasna Mwilima, Kesi hiyo imeahirishwa mpaka jumatatu Novemba 30-2015.

Kesi hiyo iliyopewa No. 2/2015 ilitarajiwa kusikilizwa leo hii katika mahakama Kuu Kanda ya Tabora ambapo Jaji wa Mahakama hiyo, Mhe Utamwa aliamua kuahilisha kesi hiyo  kwa hoja kwamba mshtakiwa wa kwanza Bi Husna Mwilima anapaswa kujibu kwanza kabla kesi haijaendelea kusikilizwa na kuamuliwa.


Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo hilo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Uvinza Eng. Lubeni Mfune, pamoja na  Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Jaji Utamwa ameagiza kesi hiyo  kusikilizwa jumatatu ili kuendana na muda uliopo kisheria ambapo kesi hii ndogo inapaswa kuamuliwa ndani ya siku14 ili kesi ya msingi iweze kuendelea.

Katika kesi hii ndogo ya awali kabla ya kesi ya msingi, mahakama itaamua kiasi ambacho Mh Kafulila atatakiwa kulipa kama gharama za dhamana ambayo kisheria kwa wastakiwa watatu wanatakiwa kulipa Tsh. milioni15.


Madai ya Kafulila katika kesi hiyo, anamlalamikia msimamizi wa uchaguzi kwa kumtangaza mgombea ambaye hakustahiri kutangazwa mana hakupata kura nyingi ila inadaiwa alifanya hivyo kwa shinikizo kutoka ngazi za juu serikalini.