Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Nov 30, 2015

WANANCHI KIGOMA WATAKIWA KUTIMIZA MASHARTI YA TASAF



WAKATI Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ukiendela na zoezi lake la ugawaji wa pesa ili kunusulu kaya maskini kwa awamu ya tatu katika Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, Wananchi katika Wilaya hiyo wametakiwa kutimiza masharti ili kutimiza malengo ya mfuko huo.

Mfuko huo unalenga kwa kila kaya inayopewa msaada kuhakikisha inazitumia pesa hizo kuwapeleka watoto shuleni sambamba na akina mama kuhudhulia klini kwa asilimia 80.

Hayo yalizungumzwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe, Simoni Mumbeye wakati akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Msagala  Wilayani humo ambapo alisema kuwa, Serikali kupitia TASAF awamu ya tatu inahitaji kuziwezesha kaya maskini ili kukidhi mahitaji ya elimu kwa watoto pamoja na akina mama wajawazito wanaotakiwa kwenda kliniki.
Wananchi wanaotoka katika kaya maskini wakigawiwa pesa katika zoezi linalofanywa na TASAF awamu ya Tatu.

Alisema kuwa, serikali inahitaji kuona hakuna kaya ambayo inashindwa kuwapeleka watoto shuleni kwasababu ya kukosa pesa sambamba na akina mama kushindwa kufika klini mara wanapohitajika kufanya hivyo.

“Kinachotakiwa kufanyika kwa wananchi ambao wameshapewa pesa ni kutimiza maagizo hayo na si vinginevyo kama ni watoto walikuwa hawaendi shule basi wapelekwe mara moja mana ndio lengo la TASAF” alisema Mumbeye.

Aidha Mumbeye alisema kuwa,  endapo kuka kaya itabainika inatumia pesa hizo kwa shughuri zingine tofauti na maelekezo ya TASAF, kaya hiyo itatolewa katika orodha na nafasi yake itapewa kaya nyingine yenye sifa.


“Wengine baada ya kupewa pesa hizo huzitumia kwa kunywa pombe au kuzitumia katika njia ambazo hazina faida kwa familia, lakini naomba mtambue kuwa kufanya hivyo ni kwenda kinyume na malengo ya TASAF” alisisitiza Mumbeye.

Kwa mujibu wa Mratibu wa TASAF wilayani humo, Deogratiasi Chubwa, jumla ya shilingi milioni 960 zilitolewa kusaidia kaya masikini katika vijiji 36 ambapo kaya elfu 8932 zilinufaika wilani hapo.

Kwa upande wao baadhi ya walengwa walionufaika na mradi huo Agripina Dagrasi na Ezekia Mfaume walisema kuwa baada ya kupokea pesa kutoka TASAF tayari wanaona mabadiriko katika familia zao kwani watoto wao kwasasa wanakwenda shule pia pesa hizo zinawasaidia katika mahitaji madogomadogo ya kifamilia.
Wananchi wanaotoka katika kaya maskini wakigawiwa pesa katika zoezi linalofanywa na TASAF awamu ya Tatu.