Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Nov 30, 2015

POLISI KIGOMA YAKAMATA RISASI 32 NA MENO 2 YA TEMBO



JESHI la Polisi mkoani Kigoma linamshikilia Meshack Mtondo (37)  mkazi wa Kijiji cha Kasanda Katika Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma kwa tuhuma za kukutwa na meno mawili ya tembo pamoja na risasi 32 za SMG ambacho ni kinyume na sheria.

Akizungumza na Blog hii leo leo hii, Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, SACP Ferdinand Mtui, alisema kuwa, tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita majira ya 7:00 mchana baada ya  askari kupata taarifa kutoka kwa wasamalia wema.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SACP Ferdinand Mtui akionyesha meno ya tembo yaliyokamatwa.
Alisema kuwa, baada ya Polisi kupewa taarifa walifika nyumbani kwa mtuhumiwa na walipofanya upekuzi walifanikiwa kukamata meno mawili ya tembo pamoja na risasi 32 vyote vikiwa ndani ya mfuko wa sandarusi.

“Juhudi za kukamatwa kwa mtuhumiwa zilichangiwa na wananchi wanaochukia uharifu ambao baada ya kubaini umilikwaji wa nyara hizo za serikali walitoa taarifa kwa Polisi waliokuwa doria na kufanikisha kukamatwa kwa mtuhumiwa” alisema kamanda Mtui.
Risasi 32zilizokamatwa nyumbani kwa Meshack Mtunda.
Aidha Kamanda Mtui alisema kuwa, Mtuhumiwa alikamatwa na taratibu za kumfikisha mahakamani zinaendelea ili akajibu mashitaka yake ya kumiriki Nyara za serikali ambacho ni kiyume na sheria pamoja risasi zile.

Hata hivyo Kamanda Mtui aliwapongeza wananchi kwa ushirikiano waliouonyesha ambao ulipelekea kukamatwa kwa mtuhumiwa pia aliwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa kwa Polisi kila wanapobaini vitendo vya kiharifu.