Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Dec 19, 2015

WAFANYABIASHARA KIGOMA WAITAKA NHIF KUWAREKEBISHIA MASHARTI



WAFANYABIASHARA mkoani Kigoma wamelitaka shirika la Bima ya Afya (NHIF) kuwarekebishia masharti ya kujiunga na mfuko huo kama ilivyo kwa wananchi walioko kwenye Taasisi na makundi mbalimbali.

Hayo yalizungumzwa katika mkutano kati ya wafanyabiashara na NHIF mkoani hapa, ambapo wafanyabiashara hao waliomba taratibu iliyowekwa ya kila mfanyabiashara kulipia kiasi cha Tshs 76000 bila kuwa na mtu hata mmoja ndani ya familia ibadilishwe ili na wao wajiunge katika mfuko huo.
Afisa Masoko wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Kigoma, akitoa mada katika semina kati ya NHIF na Wanyabiashara.
Akitoa maoni kwa niaba ya wafanyabiashara, Makamu mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara (TCCIA) mkoani Kigoma, Sethi Naftari, alisema kuwa NHIF ilitoa kipaumbele kwa wananchi walioajiliwa na walioko katika makundi mbalimbali kujiunga katika mfuko huo kwa Tshs 76000 huku wakiwajumuisha wategemezi wao katika familia.

Alisema, kwakuwa mfuko huo una lengo la kuwasaidia watanzania wote unatakiwa kuregeza masharti kwa wafanyabiashara ambao wamejiajiri wenyewe ili nao waweze kujiunga katika mfuko huo na kunufaika na matibabu pamoja na wategemezi wao katika familia.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyabiashara Mkoa wa Kigoma, Sethi Naftari, akitoa maoni kwa niaba ya wafanyabiashara.
"Ni kweli wengi wetu tulikuwa hatuna uelewa kuhusu faida za Bima ya Afya ila baada ya NHIF ktoa elimu sote tumeelimika na tunakiu ya kujiunga mana sula magonjwa halikwepeki lakini ni vyema wakalekebisha masharti yao kwetu wafanyabiashara " alisema Naftari.

Nao baadhi ya wafanyabiasha akiwemo Idd Kimenyi, Frola Jonathan na Michael Sabwebwe, walisema kuwa, elimu waliyoipata ni nzuri lakini tatizo ni upande wa malipo ya kujiunga na mfuko huo ambayo yanamfunga mfanyabiashara kujiunga na mfuko huo akiwa peke yake  licha ya kuwa ana familia.

Walisema Kuwa ili kuweka usawa kwa lengo la kuwasaidia watanzania wote ni vyema taratibu hiyo ikabadirishwa kwa watu wote bila kubagua ili na watu wao waweze kumudu gharama hiyo ambayo itawasaidia pamoja na wategemezi wao.
Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Saveli Mwangasame, wa Kwanza kushoto akiwa na Kaimu Mwenyekiti wa Wafanyabiashara (TCCIA) mkoa wa Kigoma, Sethi Naftari wakisikiliza mada zinazotolewa na Viongozi wa NHIF Mkoani Kigoma.
“Mimi nina mke na watoto lakini NHIF inasema natakiwa kujiunga peke yangu tena kwa pesa nyingi jambo ambalo linakuwa ngumu kwangu, sasa kama wa wanahitaji kutusaidia basi wapunguze ada ya kujiunga iwe chini ya Tsh. 76000 au waache hiyo hiyo lakini watuache tuwajumuishe wategemezi wetu katika familia kama ilivyo kwa waajiriwa na watu kutoka makundi mbalimbali” alisema mmoja Michael Sabwebwe.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa NHIF mkoani Kigoma, Emmanuel Antony alisema kuwa kwasasa wanatoa elimu katika makundi mbalimbali kufahamu faida za mfuko wa Bima ya Afya ndio mana waliamua kuongea na wafanyabiashara.

Alisema kuwa, kwa wale ambao wameelewa umuhimu wa kuwa na uhakika wa matibabu muda wowote hawatojari gharama ya kujiunga kwani suala la kuugua ni la kila mtu na mtu anaweza kuugua Muda wowote hivyo kama ana Bima ya Afya atatibiwa bure hata kama ugonjwa wake unagharimu pesa nyingi hadi kupona.
Baadhi ya wafanyabiashara mkoani Kigoma walioshiriki katika mkutano kati ya NHIF na wafanyabiashara kwa lengo la kupata elimu.
Baadhi ya wafanyabiashara mkoani Kigoma walioshiriki katika mkutano kati ya NHIF na wafanyabiashara kwa lengo la kupata elimu.