Mshambuliaji Lionel Messi ameibeba Barcelona baada ya kufunga mabao matatu
katika mchezo dhidi ya Granada na kuiwezesha timu yake kurudi kileleni mwa ligi ya La Liga.
Messi aliiweka Barcelona kifua mbele baada ya kupata pasi nzuri kutoka kwa mshambuliaji matata wa timu hiyo Louis Suarez na aliongeza bao la pili katika dakika ya 58 kabla ya Neimar kufunga bao la nne.