Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Aug 9, 2016

ZUIO LA NAFAKA KUUZWA NJE YA NCHI WATOLEA UFAFANUZI

Nafaka za mahindi ni moja ya nafaka zilizozuiliwa kuuzwa nje ya nchi.


Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Samson Anga (Kushoto) akiwa na Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma, Charles Pallangyo (kulia).
Serikali ya mkoa wa Kigoma imewataka wananchi kutambua kuwa bidhaa zilizozuiliwa kuuzwa nje ya nchi ni Nafaka za Mahindi, Unga, Mchele, Mihogo na Mpunga na si kama ilivyonukuliwa kwa bidhaa zingine ambazo hazijatajwa.

Ufafanuzi huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga alipozungumza na waandishi wa habari hivi karibuni baada ya kuenea kwa uvumi kuwa serikali imezuia uuzwaji wa bidhaa zote za chakula kwenda nje ya nchi kama  Congo, Burundi na Rwanda.

Bwana Anga amesema kuwa bidhaa kama Viazi, Matunda ya aina zote pamoja na mboga mboga hizo zote zinaruhusiwa kuuzwa nje ya nchi hivyo taarifa zilizoenea kuhusu kuzuliliwa kwa bidhaa hizo sio kweli hivyo wananchi waendee kuuza bidhaa zao.

"Bidhaa hizo ziendelee kuuzwa bila woga ila kwa nafaka kama zilivyotajwa hizo ndio zimezuiliwa ili kufanya tathimini ya kiasi cha nafaka kilichopo" alisema.

Aidha Anga amesema, kiliundwa kikosi kazi kwaajiri ya zoezi hilo ambalo limeshakamilika hivyo muda si mrefu taarifa itatolewa ili kuendelea na uuzaji kama kawaida .

Hata hivyo Anga amesema wametoa maelekezo kwa wakuu wa Wilaya wote mkoani Kigoma  kusitisha Zuio la Bidhaa tofauti na zilizozuiliwa na Wizara ya Kilimo na Uvuvi na Mifugo.