Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 9, 2016

VIJANA WANAOMALIZA MAFUNZO YA JKT WATAKIWA KULINZA AMANI NA USALAMA WA NCHI


Mkuu wa Mkoa Kigoma Issa Machibya (Mwenye suti) akikagua gwaride la vijana wa kujitolea Operesheni Kikwete  katika kambi ya Jeshi la kujenga Taifa Bulombora wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma wakati wa sherehe ya kumaliza mafunzo kwa vijana 528 wa kujitolea.
Makamanda wa gwaride wakiwaongoza washiriki wa mafunzo ya kujitolea katika kambi ya JKT Bulombora kutoa heshima kwa mwendo wa kasi kwa Mkuu wa mkoa Kigoma (Hayupo Pichani) wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo hayo yanayojulikana kama Operesheni Kikwete.

Vijana wameomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)  wametakiwa kutumia mafunzo waliyopewa kwa kushirikiana na jamii kwa kuwafichua waharifu na wahamiaji haramu na kuongoza juhudi za kuimalisha usalama katika maeneo ya nchi kwa kushirikiana na jeshi la polisi nchini chini ya farisafa ya polisi jamii na ulinzi shirikishi.

Akizungumza katika sherehe za kufunga mafunzo kwa vijana 528 yanayojulikana kama Operesheni Kikwete katika kambi ya JKT Bulombola Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Mstaafu Issa Machibya, aliwataka vijana hao kujari masrahi ya Taifa badara ya kujiingiza katika makundi ya uharifu ambayo huleta hasara kwa taifa.

Alisema, vijana ndio uti wa mgongo wa Taifa hivyo wanawaangaliwa kwa jicho tatu hasa katika kudumisha amani ya nchi.

Aidha Machibya, aliwataka vijana hao kuwa mfano bora miongoni mwa vijana wanaowazunguka katika maeneo yao hasa kwa kujiletea mafanikio kupitia mafunzo waliyoyapata.

Awali akisoma risala kwa niaba ya washiriki wenzake wa mafunzo hayo, Gloria Kishai, amesema,  sambamba na kujivunia kupata mafunzo hayo watayatumia  kwa manufaaa ya taifa sambamba na kujituma katika kazi za kimaendeleo.