Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 15, 2016

WAKUU WA SHULE KIGOMA WALALAMIKIA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI BAADA YA MICHANGO KUFUTWA



Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari mkoani Kigoma wamezungumzia chamgamoto zinazowakabiri baada  ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzuia michango kwa wazazi kwa lengo la kutoa elimu bure.

Wakizungumza blog hii Wakuu wa shule hizo wamesema, Changamoto hizo zimeanza kuonekana baada ya serikali kutoa pesa kwa kila shule ambapo  uchache wa pesa hizo unasababisha kushindwa kukidhi mahitaji ya shule zao kama ilivyokuwa awali.

Thomas Masama ambaye ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Mjini, amesema, tangu kuzuiliwa kwa michango ya wazazi shughuri mbambali za uendeshaji wa shule umekuwa mgumu kutokana na pesa zilizotolewa kuwa chache.

Amesema, kwasasa wanashindwa kununua vifaa vya shule, kuendesha vikao vya bodi  sambamba na  kuwalipa walinzi mishahara yao pia bado shule ina madeni ambayo ilichukua vifaa kipindi pesa hazipo.

“Shule yangu ilipewa Tsh. 286,000/= ambapo pesa hiyo haitoshi kulingana na mahitaji tuliyonayo na kwa wingi wa wanafunzi nilionao ambao ni 540  ilitakiwa nipewe kiasi cha Tsh. 5,040,000/= kwani Waziri wa Elimu alisema kila mwanafunzi analipiwa Tshs, 10,000/=” alisema Mwalim Msama.

Nae Mkuu wa Shule ya Sekondari  Hwazi, Jonathan Nkundike, amesema, baada ya michango kufutwa na kupokea pesa kutoka serikalini changamoto kubwa inayoikumba shule yake ni kushindwa kuwalipa mishahara wasaidizi na walinzi wa shule ambao waliajiriwa na shule.

Ameongeza kuwa, katika uendeshaji wa shule kuna vifaa mbalimbali huwa vinahitajika sambamba na uendeshaji wa vikao vya bodi  hivyo kwasasa wanashindwa wafanye kipi kutokana na pesa kuwa chache kutokana na mahitaji ya shule kwa ujumla.

“Tunaweza kusema tununue  vifaa vya shule ambavyo ni muhimu ila bado vikao vya bodi navyo  ni muhimu mana bodi ya shule ndio imepewa dhamana ya kusimamia pesa hizo pia  walinzi na wasaidizi wa shule wanadai pesa zao na mwisho wa siku wataondoka mana hawawezi kufanya kazi bila kulipwa hivyo shule inaweza kubaki bila walinzi na wasaidizi” amesema Nkundike.

Hata hivyo walimu hao wameitaka  serikali kuangalia upya suala hilo na kama imedhamilia kutoa elimu bure basi itoe pesa za kutosha sambamba na kutoa  vifaa vya shule kama madaftari, chaki, vitabu, pia kutenga mishahara kwaajiri ya walinzi wa shule ili kutatua changamoto zinazozikabili shule hizo baada ya michango kufutwa.