Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 28, 2016

WANANCHI KIGOMA WAPINGA KAULI YA SERIKALI



Waziri wa habari Utamaduni na Michezo Nape Nnauye.
Kauli ya serikali ya kuzuia vipindi vya bunge kurushwa moja kwa moja kwenye runinga imepokewa kwa muono tofauti na wakazi wa Kigoma baada ya kuonekana haina tija kwa wananchi.

Wakitoa maoni yao kwa nyakati tofauti wananchi hao wakiwemo viongozi wa dini mkoani humo wameonyesha kutoridhishwa na kauli ya serikali inayoelekea kuwanyima wananchi uhuru wa kupata habari kwa muda muafaka.

Shaban Guoguo ambaye ni Shekhe Mstaafu wa Mkoa wa Kigoma, amesema, kilichoamuliwa na serikali ni upindishwaji wa sheria mana bunge ni la wananchi na sio la serikali hivyo wananchi wanataka kuona wabunge wakiwasilisha yale waliyowatuma.

Amesema, kama serikali inatambua bunge ni la wananchi na yanayozunguzwa humo ni kwaajiri ya kutetea taifa basi mambo yote yawe wazi na kama wanaamua kuzuia wananchi wasione basi haina haja kuwa na bunge mana itaonekana yanayozunguzwa humo ni maovu hivyo wanayaficha yasionekane na wananchi.

“Serikali inataka kuleta mgogoro usio na sababu, kama bunge linavurugu, wabunge hawaelewani na nidhamu haipo mbungeni, dawa si kuzuia wananchi wasione mana kuzuia si kutatua tatizo mana sasa kama wamezuia kabisa itafika siku wabunge watapigana kabisa mana wanajua hawaonwi na waliowatuma” amesema Shekhe Guoguo.

Nae Mthibiti  Ubora wa Shuke mkoani Kigoma, Romward Nyuki amesema, serikali imeamua kuvunja haki ya binadamu ya  kupata taarifa sahihi mana lengo lao ni kuonyesha vipindi vilivyo recodiwa ambavyo kimsingi vinakuwa vimechunjwa kwa kuondoa mabaya yote.

Amesema, bunge linakaa kwa masaa manane kwa siku ila serikali inataka matukio yote yaonyeshwe kwa saa moja ambapo itawalazimu kuondoa vitu vingi jambo ambalo litaua dhana nzima ya wananchi kufahamu kinachoendelea bungeni.

“Serikali itambue kuwa ikiendelea kung’ang’ania suala hilo basi ijue wananchi watapoteza imani na serikali yao na kuamini kuwa bunge halipo kwaaajiri ya masrahi ya wananchi bali kwa masrahi ya watu wachache” amesema Nyuki.

Gidion Ruhadha ambaye ni Kaimu Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mnarani, amesema, serikali inatakiwa kutambua matokeo ya kauli yake kama yanafaida kwa taifa au kwa watu wachache hivyo jambo la msingi ni kujali mahitaji ya wananchi .

“serikali inayoongozwa na sera ya ukweli na uwazi ndio hufanikiwa mana hutoa uhuru kwa watu wote kufahamu mambo yanayoendela katika nchi yao sasa kama wameamua kuficha basi hatuna budi kusema wanataka wapate fursa ya kuwagandamiza wananchi ili wajinufaishe wenyewe” amesema Ruhaza