Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 4, 2016

WANANCHI KIGOMA WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA SERIKALI ILIYOKO MADARAKANI




Wananchi mkoani Kigoma wametakiwa kuachana na tofauti za kiitikadi zilizojitokeza kipindi cha uchaguzi uliofanyika Octoba 25 mwaka jana na kuungana na serikali iliyopo madarakani katika kuiombea  utumishi uliotukuka.



Akizungumza  katika mkutano wa kumshukuru Mungu kwa kufanikisha zoezi la uchaguzi kuisha kwa amani na utulivu uliofanyika Desemba 30, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kanali Mstaafu Issa Machibya alisema, wananchi wote wanatakiwa kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuri  kwa kauli yake ya HAPA KAZI TU kwa  kufanya kazi kwa bidii kama anavyoagiza.
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Mstaafu Issa Machibya akizungumza na wananchi katika ibada ya kumshukuru Mungu iliyofanyika katika viwanja vya Community Centre katika Manispaa ya Kigoma-Ujiji.
Alisema, wananchi wote wanatakiwa kutoa ushirikiano kwa viongozi mbalimbali waliochaguliwa kuanzia ngazi ya mtaa, kata, Wilaya na Mkoa bila kujari tofauti za kiitikadi, kidini na kikabila.


Aidha Machibya aliwataka wananchi kuendelea na utulivu ili Tanzania iendelee kuitwa kisiwa cha amani badala ya kuanzisha fujo ambazo zitapelekea kuipoteza amani ilipo.



“Nahitaji wananchi wote muelewe kuwa huu sio muda wa marumbano bali ni muda wa kufanya kaza kwa bidii kwa lengo la kuziendeleza familia zetu na nchi kwa ujumla” alisema Machibya.
Askofu Mstaafu wa Kanisa la Pentekoste Assembles Of God Tanzania (P.A.G.T) Kigoma, Michael Kulwa akisoma risala kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Issa Machibya,  kwa niabaya ya Wachungaji wa makanisa ya Kikristo mkoani Kigoma.

 Akisoma risala kwa niaba ya Umoja wa Makanisa ya Kikristo  (CPCT) mkoa wa Kigoma, Askofu Mstaafu wa  Kanisa la Pentekoste Assembless Of God Tanzania (P.A.G.T.) Kigoma, Michael Kulwa, alisema kuwa, amani iliyoko sasa mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi inatokana na utulivu wa watanzania sambamba na maombi ya wakristo waliojitoa kuuombea uchaguzi uishe kwa amani.



Kulwa alisema kuwa, ni wakati sasa kwa viongozi wote wa idara mbalimbali, wanasiasa na wananchi wote kwa ujumla kuwa, sasa uchaguzi umekwisha, ni vyema wote kuungana kwa pamoja na kuwa kitu kimoja kwa kutunza amani ya nchi na kutekeleza yale yanayoagizwa na Rais Magufuri.



“Tunafahamu kuwa Watanzania wote wanajua yanayotokea nchi za jirani mara wanapomaliza chaguzi zao ambapo amani hutoweka na nchi kuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe hivyo ni vyema sisi watanzania kuendelea kumuomba Mungu azidi kutupa moyo wa upendo kwa kila mmoja wetu ili amani iendelee kudumu” alisema Askofu Kulwa.