Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 2, 2016

WAZIRI MKUU AIONYA SUMATRA KIGOMA




Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, akizungumza na wanannchi alipokuwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Kigoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, amekemea tabia ya Mamlaka ya Usafirishaji wa Nchi kavu na Majini (SUMATRA) ya kuwatoza wavuvi ushuru kwa njia ya dora.

Akizungumza na wavuvi baada ya kufungua soko jipya la samaki, liloko Kata ya Kibirizi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani hapa, Waziri Mkuu alisema, licha ya kupokea malalamiko kutoka kwa wavuvi kuhusu tozo ya dora suala hilo ni kinyume na sheria.

Alisema, tozo la dora hufanyika kwa watu ambao si raia wa nchi hii lakini kwa Watanzania wote wanatakakiwa kutumia pesa ya Kitanzania ambayo ni rahisi kupatikana.

Aidha Waziri Mkuu aliitaka SUMATRA kuacha tabia hiyo ili kuepusha migogoro isiyo na tija baina  yao na Wananchi.

Awali wavuvi wanaotumia Ziwa Tanganyika walilalamikia usumbufu wanaoupata wa kubadirisha pesa za Kitanzania kuwa dora ili kulipia ushuru baada ya kutakiwa kufanya hivyo na SUMATRA.

Hata hivyo Waziri Mkuu alimaliza Ziara yake ya siku tatu mkoani kigoma hapo jana ambapo alitembelea Wilaya tatu ikiwemo Kigoma mjini, Kasulu na Kibondo.