Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Feb 8, 2016

KITUO MAALUMU CHA POLISI CHAKOSA HUDUMA YA VYOO


Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, SACP Ferdinand Mtui.

Jeshi  la Polisi Mkoa wa Kigoma limetakiwa kutatua kero ya ukosefu wa vyoo katika kituo cha ukaguzi wa magari kilichopo njia panda ya Mwandiga ambapo huwalazimu askari kujisaidia vichaka mara wanapohitaji kufanya hivyo.

Akizungumza na blog hili hapo jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha NRA Taifa, Fadhili Kiswaga , alisema kuwa,  Askali hufanya kazi ya kulinda raia na mali zao jambo ambalo huwafanya baadhi ya Askali  kuwa katika maeneo magumu.

Alisema kuwa, eneo la njia panda ya Mwangida ni eneo muhimu sana kwa magari kukaguliwa kutokana na njia hiyo kuwa ya kutoka na kuingia mkoani  Kigoma ambapo Askali waliweka kituo kwaajiri ya ukaguzi hivyo Askali huwepo eneo hilo masaa 24 ili kukagua usalama wa magari yanayoingia na kutoka.

“Licha ya kuwa eneo hilo ni muhimu sana na askali huwepo muda wote lakini eneo hilo halina vyoo kwaajiri ya kujisaidia pindi askali wanapotaka kufanya hivyo, kukosekana kwa vyoo huwafanya askari kujisadia vichakani na kwenye mashamba ya watu” alisema Kiswaga.

Aidha Kiswaga alisema kuwa, kitendo cha askari katika kituo hicho kujisaidia vichakani ni cha uzalilishaji na kinaonyesha jeshi la polisi haliwajari askali wake wanapokuwa katika maeneo ya kazi.

“Jeshi la polisi linatakiwa kujenga vyoo katika eneo hilo ili kuonyesha linawajari askali wake wanapokuwa katika maeneo ya kazi” aliongeza Kiswaga.

Alipoulizwa kuhusu kero za vyoo katika eneo la njia panda ya Mwandiga, Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, SACP Ferdinand Mtui, alikili kuwepo kwa kero hiyo na aliongeza kuwa atazungumza na wahusika wa utawala ili kutatua kero hiyo kutokana na kituo hicho kuwa kikubwa.

“Nawataka Askali waendelee kuzingatia kanuni na sheria za kazi kwa kuhakikisha  wanafanya ukaguzi kwa magari yanayoingia na kutoka mkoani hapa na suala la vyoo litafanyiwa kazi ili huduma hiyo ipatikane haraka iwezekanavyo” alisema Kamanda Mtui.

Kwa upande wa baadhi ya Askari wa usalama barabarani  ambao hukaa katika kituo hicho cha ukaguzi, majina yao yanahifadhiwa, kwa nyakati tofauti walikili kuwepo kwa tatizo la ukose vyoo linalowasumbua kwa muda mrefu sasa.