Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

May 1, 2016

NEWCASTLE YAPAMBANA KUBAKI LIGI KUU

Klabu ya Newcastle imaimarisha matumaini yake ya kusalia katika ligi kuu ya Uingereza kufuatia bao la Andros Townsend na penalti iliopanguliwa na kipa wa kilabu hiyo dhidi ya Crystal palace.

Huku Norwich ikicheza dhidi ya Arsenal na Sunderland kutoka sare na Stoke,Newcastle sasa imepanda hadi nafasi ya 17 na kuondoka katika eneo la kushushwa daraja.

Towsend aliipatia Newcastle bao la kwanza baada ya mapumziko kupitia shambulio kali.
Kipa Darlow baadaye aliokoa Newcastle alipookoa penalti ya Yohan Cabaye.