Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Aug 11, 2016

ONGEZEKO LA BEI YA USAFIRISHAJI WA DAGAA LAWATESA WAFANYABIASHARA KIGOMA



Wafanyabiashara wa dagaa Manispaa ya kigoma ujiji wameilalamikia serikali kwa kuongeza  gharama za usafirishaji wa dagaaa kutoka Tsh 170 hadi Ths 2200 kwa kilo moja jambo linalofanya mauzo ya dagaa kushuka hasa kwa mauzo ya nje ya nchi.

Wafanyabiasha hao wamesema serikali imefanya maamuzi ambayo yanawakandamiza katika biashara kutokana na ongezeko hilo kuwazuia wateja kutoka nje kushindwa kununua bidhaa hiyo.

Aidha Wafanyabiashara hao wameitaka serikali kuwa na tabia ya kuwashirikisha wananchi katika mabadiriko yanayogusa uchumi wao.

Akizungumzia malalamiko ya wauza dagaa mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga amekiri kuwepo kwa ongezeko la Gaharama za usafirishaji huku akiongeza kuwa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuni inafanya marekebisho baada ya kugundua ongezeko hilo lilifanyika kimakosa.