Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Aug 6, 2016

SOKO LA UJIRANI MWEMA LATAKIWA BUHIGWE ILI KUKUZA UCHUMI



Serikali imetakiwa kujenga miundombinu katika mpaka uliopo kata ya Muyama Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma na nchi jirani ya Burundi hasa soko la ujirani mwema ili kuwawezesha wananchi kuuza na kufanya biashara zao kwa uhuru na kujiletea maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Diwani wa Kata ya Muyama, Abdala Moshi wakati akizungumza na Radio Joy ambapo amesema kutokana na Kata a Muyama kuwa mpakani mwa nchi ya Burundi kumepelekea raia wa nchi hizi mbili kuwa na muingiliano wa  kibiashara.

Amesema endapo serikali ikijenga soko la ujirani mwema litatoa fursa kwa watanzania wa kata hiyo kuuza bidhaa zao kwa wingi na kujiingizia kipato pia kuingizia nchi pesa za kigeni.

Hata Hivyo Moshi alisema awali kulikuwa na mkakati wa kutengeneza soko la ujilani mwema kabla ya Wilaya ya Buhigwe kupewa hadhi ya Wilaya lakini mkakati huo ulikwama baada ya kugawa Wilaya.

Kwa upande wao wananchi wa kata hiyo, akiwemo Abu Ahmad na Ndimugwanko Gwimo waliitaka serikali kuboresha soko lililopo ili kutoa fursa kwao kuuza bidhaa nyingi jambo litakalowafanya kujiingizia kipato.