Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Aug 12, 2016

TELEZA AKAMATWA KIGOMA WANANCHI WAMPA KIPIGO KIKALI


Kijana ambaye alivamia nyuma ya Mwanamke mmoja na kutaka kumbaka, akiwa hajitambui baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira.

Kufuatia matukio ya baadhi ya wanawake kuingiliwa kimwili bila ridhaa yao nyakati za usiku na watu wanaojulikana kwa jina la TEREZA Mtu mmoja ambaye jina lake halijafahamika amekamatwa na Wananchi wakati akijaribu kumuingilia Mwanamke mmoja katika kata ya Mwanga kusini Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Akisimulia tukio hilo Ramadhani Habibu mkazi wa mtaa wa Vamia katika kata hiyo ambaye ndiye aliyepambana na TEREZA huyo amesema, Mtu huyo aliingia kwenye chumba cha mke wa kaka yake na kutaka kumbaka lakini baada ya shemeji yake kupiga kelele za kuomba msaada alitoka na kwenda kupambana na mtu yule.

“Baada ya kusikia shemeji akiomba msaada nilitoka nikiwa na kipande cha nondo nilipoingia chumbani kwa shemeji yangu nikamkuta mwanaume akiwa amevaa chupi tu akitaka kumbaka na kwakuwa nilikuwa nanyemelea hakuniona ndio nikampiga na kile kipande cha nondo shingoni” alisema Habibu.

Aidha Habibu aliongeza kuwa baada ya kumpiga nondo mtu yule alipata mshituko hivyo akatumia mwanya huo kupambana nae na baada ya muda majirani walikuja na kuanza kumshambulia kabla ya Polisi kufika na kumpeleka kituoni.

Kwa upande wa  Mwanamke ambaye ndie alivamiwa na mtu huyo amesema, kabla ya kulala alifunga mlango wa balazani lakini mlango wa chumbani alisahau kuufunga na ilipofika saa kumi usiku TEREZA huyo akaingia na kutaka kumbaka.
Kijana ambaye alivamia nyuma ya Mwanamke mmoja na kutaka kumbaka, akiwa hajitambui baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira.
 “Wakati nimelala nilisikia mtu ananipapasa akinivua nguo ya ndani ndipo nikashtuka na kumuuliza ni nani, akanambia nikae kimya ndipo nikaanza kupiga kelele za kuomba msaada baada ya muda shemeji yangu akaja na kumpiga nondo hapohapo wakaanza kupigana majirani walipokuja wote tukaanza kumpiga” alisema Mwanamke huyo.

Nae Afisa Mtendaji wa Kata hiyo Mwamvita Jumanne aliitaka  serikali kulihimiza jeshi la polisi kuwa na utaratibu wa kufika mapema kwenye matukio ya uharifu baada ya kupewa taarifa kutokana na wao kufika kwenye tukio saa 2 asubuhi wakati taarifa walipewa toka saa 12 alfajiri.

Akithibitisha kukamatwa kwa Mtu huyo Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma Naibu Kamishina Ferdinand Mtui amesema, baada ya mtuhumiwa kukamatwa amefikishwa mahakamani ili kujibu mashtaka yanayomkabiri.