Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Sep 8, 2016

MGANGA WA KITUO CHA AFYA JANDA KIGOMA ATUHUMIWA KWA WIZI WA PESA




Baada ya mganga mkuu wa Kituo cha afya Janda kutuhumiwa kuchukua zaidi ya shilling millioni moja kinyumke na taratibu,  mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Buhigwe ametakiwa kuchukua hatua dhidi ya mganga huyo.

Mganga huyo anaejulikana kwa jina la Dr.Froliani Asten  anatuhumiwa kwa kugushi mhatasari wa kikao cha bodi ya afya ya kata na kuchukua pesa ya mfuko wa afya ya jamii CHF ya kituo hicho

Diwani wa kata ya Janda  Bw. Pascal Nkeyemba amezungumza hayo na Radio Joy kwa njia ya simu na kusema kuwa mganga huyo aliwasahinisha wajumbe wa bodi ambao si halali na pesa zilizochukuliwa zilikuwa kwa lengo la kununua dawa ambazo hata hivyo hazikununuliwa.

Amesema amekuwa akifuatilia suala hilo katika halmashauri ili hatua ziweze kuchukuliwa lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika jambo ambalo limemfanya kumtaka mkurugenzi kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mganga huyo.

kwa upande wake mkurugenzi wa wilaya ya Buhigwe Bw.Anosta Nyamoga amekili kuwepo kwa tatizo hilo ambapo amesema limesababishwa na usimamizi mbovu katika kituo hicho na ameunda tume kuchunguza suala hilo ambayo imekamilisha kazi yake na  wakati wowote itatoa taarifa na hatua za kisheria zitachukuliwa.

Nae Mganga mkuu wa kituo cha afya cha Janda Dr. Frolian Asten amekanusha tuhuma hizo na kueleza kuwa pesa hiyo ni ya muda mrefu na bado ipo kwa mkurugenzi ambaye ndie mwenye taarifa zote.