Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Sep 8, 2016

WATOTO NANE WAFARIKI DUNIA BAADA YA KUUNGUA MOTO NDANI YA NYUMBA


Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma Naibu Kamishina Ferdinand Mtui akiongea na waandishi wa habari

Watoto nane wamefariki Dunia katika kijiji cha Chakulu, Kata ya Uvinza Tarafa ya Nguruka Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma baada ya nyumba waliyokuwemo kuungua moto.

Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Naibu kamishina Ferdinand Mtui ametoa taarifa hiyo mapema wiki hii ambapo amesema tukio hilo limetokea Septemba 4 mwaka huu majira ya saa saba usiku wakati wazazi wa watoto hao wakiwa hawapo nyumbani.

Kamanda Mtui amesema Nyumba iliyoungua ni mali ya Bw. Samike John ambaye ni mkazi wa Kitongoji cha tandala  eneo la kona nne katika kijiji hicho pia kati ya watoto waliofariki wawili ni watoto wake huku wengine wawili wakiwa ni wa dada yake sambamba na watoto watatu wa jirani yake.

Aidha kamanda mtui amesema tukio hilo limetokea wakati wazazi wa watoto hao wakiwa hawapo nyumbani ambapo moto huo ulisababishwa na jiko lililokuwa ndani.

Hata hivyo kamanda mtui amewataka wazazi na walezi kujari maisha ya watoto wao kwa kuwaaacha chini ya uangalizi wa watu wakubwa ili kuepusha matukio yoyote yanayopelekea vifo na majeraha kwa watoto.