Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Sep 8, 2016

WAHAMIAJI 1026 WAKAMATWA KIGOMA


Baadhi ya wahamiaji waliokamatwa mkoani kikgoma wakiwa katika ofisi za uhamiaji mkoa.
Baadhi ya wahamiaji waliokamatwa mkoani kikgoma wakiwa katika ofisi za uhamiaji mkoa.

Idara ya Uhamiaji mkoani Kigoma imekamata Jumla ya Wahamiaji haramu 1026 walioingia na kuishi nchini kinyume cha sharia baada ya kufanya msako katika kipindi cha mwezi April hadi Julai.

Akitoa taarifa hiyo ofisini kwake hivi karibuni, Afisa Uhamiaji Mkoani Kigoma, Naibu Kamishina Maurice Kitinusa, amesema Msako huo umefanyika katika wilaya zote mkoani hapa na wahamiaji hao ni kutoka nchi za Burundi, Congo, Rwanda, Kenya, Msumbiji na Uturuki.

Aidha Kitinusa amesema katika idadi hiyo wapo watanzania ambao wao wamekamatwa kwa kosa la kuwaficha wahamiaji sambamba na kuwazuia maafisa uhamiaji kufanya kazi yao.

Ameongeza kuwa,  watanzania wenye nia ya dhati ya kulinda nchi yao wanatakiwa  kushirikaiana na idara ya uhamiaji kwa kutoa taarifa kwa viongozi wa serikali mara wanapomuona mtu na kumtilia shaka pia amewataka watanzania kuacha kuwahifadhi watu hao mana kwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.