Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jan 13, 2017

ZAIDI YA NYUMBA TISA ZAEZULIWA NA UPEPO WA KIMBUNGA KIGOMA


Zaidi kaya tisa katika kijiji cha Muyegela wilaya ya Buhigwe mkoa wa Kigoma hazina makazi ya kuishi mara baada ya kukumbwa na kimbunga kilali kilichoezua  nyumba zao, kuharibu mazao sambamba na migugo kufa.

Wakazi hao akiwemo Silvesta Joseph amesema majira ya saa tano asubuhi upepo mkali ulivuma kijijini hapo ambapo familia nyingi zilikuwa mashambani huku wengine wakikubwa na upepo huo ambao uliezua  mabati, mifugo kufa,mazao kuharibika, nguo na vifaa mbalimbali vilivyokuwa ndani.

Aidha walitoa ombi kwa serikali ya kijiji na wilaya kuwasaidia vifaa vya ujenzi ili wamudu kukarabati nyumba zao na waweze kuondokana na adha wanazozipata za jua kali na mvua kutokana na nyumba zao kuezuliwa mabati.

Akitoa takwimu za uharibifu huo mtendaji Alphonce Ntatiye amesema kutokana na tukio hilo wao kama serikali ya kijiji kwa kushirikiana na wananchi wa maeneo hayo watashiriki kwa pamoja kuwapatia msaada waliokumbwa na adhari za kimbunga kwenye kaya zao.

Hata hivyo kamati ya ulinzi na usalama ikiongonzwa na mwenyekiti wa kamati hiyo mkuu wa wilaya Buhigwe kanal Marco Gaguti hakusita kutoa pole kwa wakazi hao na kuahidi kuwapatia msaada ili wapate maeneo mazuri ya kuishi.