Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Apr 2, 2017

MWANAMKE ANUSURIKA KUKATWA ULIMI KIGOMA


Bi Domitila Muhoza (53) mkazi wa  masanga Manspaa ya Kigoma Ujiji akiwa amelazwa katika Hospitali ya Mkoa ya  Rufaa Maweni mkoani Kigoma baada ya kuvamia na kunusurika kukatwa ulimi.
Mwanamke  mmoja ajulikanae kwa jina la  Domitila Muhoza (53) mkazi wa  masanga Manspaa ya kigoma ujiji  ameshambuliwa na mtu asiyejulikana  baada ya kuvamiwa akiwa na nia ya kumkata ulimi majira ya alfajiri  wakati akielekea kanisani.

Akizungumza na blog hii Bi Muhoza amesema wakati akielekea kanisani alisikia mtu akimshika kwa nyuma na kuanza kumpiga maeneo ya usoni na kutaka kumkata ulimi huku akimuomba pesa na vitu vingine vya thamani alivyokuwa navyo.

“Wakati akiendelea kunipiga aliingiza mkono mdomoni ili anikati ulimi, kilichonisaidia nilimng’ata meno ndio akanichia, licha ya kuwa alikuwa ameshaniumiza sana usoni na mdomoni na kuniambia nimpe pesa lakini sikuwa nazo nikamuachia nguo nilizokuwa nazo” alisema Bi Muhoza.

Aidha Bi Muhoza alisema kuwa, hakumtutambua mtu Yule kwasababu alikuwa ameshaumia ambapo baada ya mtu Yule kukimbia walikuja watu na kumsaidia kumpeleka hospitali ya Rufaa ya mkoa Maweni kwaajiri ya matibabu.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Maweni Daktari Fadhili kibaya, amesema walimpokea mama huyo akiwa na hari mbaya akivuja damu mdomoni huku akiwa na majeraha sehamu za usoni ambapo alipatiwa matibabu.

“Ulimu na sehemu zingine zenye majeraha zilishonwa na kupewa dawa na mpaka sasa amelazwa akiuguza majeraha yake, Pia hakuna athari kubwa aliyoipata kwenye ulimi hivyo tunategemea baada ya muda ulimi utapona na kuanza kufanya kazi kama kawaida” alisema Daktari Kibaya.

Nae Lovenes Lauson ambaye ni mkwe wa Bi Muhoza alisema walipigiwa siku na kuambiwa mama yao amevamiwa na majambazi, wakaamua kwenda eneo la tukio na kumkuta ana hali mbaya ndipo wakamchukua na kumpeleka Polisi kwaajiri ya PF 3 na hatimaye wakampeleka Hospitali.