Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Apr 5, 2017

MACHINJIO YA UJIJI KIGOMA YAFUNGWA


Watu wanaofanya shughuli ya kuchinja wanyama katika machinjio ya Ujiji mkoani Kigoma wakiendelea na shughuli hiyo kabla ya kufungwa kwa machinjio hiyo.

Manispaa ya Kigoma ujiji imesaria na machinjio moja inayopatikana Ujiji ambayo hata hivyo haikidhi mahitaji ya wakazi wa manispaa hiyo, hii ni kufuatia  Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini -TFDA kanda ya magharibi kufunga machinjio ya  kibirizi kutokana na kuwa na miundombinu mibovu inayohatarisha afya ya binadamu.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya TFDA kupokea malalamiko kutoka kwa  wachinjaji wa machinjio hiyo kuhusu ukosefu wa maji jambo lililomfanya Meneja wa TFDA Kanda ya Magharibi Edgar Mahundi kufika katika eneo hilo na kujionea hali  ya  miundombinu  ilivyo chakavu jambo lililomfanya kufunga machinjio hiyo.

Kwa upande wao wachinjaji na wanunuzi wa jumla kwenda mabuchani wamesema kuwa kwa kawaida  ruzuku ya serikali na ushuru wanaolipa wafanyabiashara ungetakiwa kurekebisha machinjio hiyo lakini hakuna kinachofanyika.

“Ni jambo la ajabu serikali kushindwa kurekebisha machinjio hiyo licha ya kuwa kila siku michango ya ushuru na kodi za wananchi zinakusanywa sasa ka ni hivyo pesa zile zinaenda wapi?” waliuliza.

Naye mkuu wa idara ya uvuvi na mifugo manispaa ya kigoma Ujiji dr John Shauri ameonyesha kupokea hatua hiyo kwa mshituko huku akisisitiza kuwa tatizo ni ufinyu wa bajeti huku akibainisha kuwa tayari kuna pesa imetengwa kwaajiri ya  kuboresha machinjio hiyo.