Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Apr 10, 2017

WAFANYABIASHARA KIBONDO WALALAMIKIA KUPANDA KWA USHURU

Wafanyabiashara na wakulima wilayani Kibondo mkoani Kigoma wameulalamikia uongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo kutokana na ongezeko la bei za ushuru wa bidhaa hali inayopelekea  wanunuzi kutoka nje ya wilaya waliokuwa wakifuata mazao ikiwemo mahindi na maharage, kuacha kununua bidhaa hizo kwa kile kinachodaiwa ni kutokana na bei za ushuru kuongezeka.

Wakizungumza na waandishi wa habari siku chache ikiwa ni baada ya wafanyabiashara na wakulima hao kuandamana katika ofisi za jumba la maendeleo mjini kibondo, wamesema ushuru umepanda kutoka shilingi elfu moja mia tano hadi elf mbili na kufikia elfu sita kwasasa bei hiyo ikiwa ni kwa mfuko wa debe sita hali ambayo imewafanya wauze bidhaa hizo kwa mda mrefu tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Wamesema licha ya kutumia jitiahada zao za kujikwamua kimaisha kupitia biasharana na kilimo, hali ya mzunguko wa fedh aimekuwa ngumu kutokana na kitendo cha halimashauri hiyo kupandisha bei za ushuru wa mazao.

Kwaupande wake kaimu mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya wilaya ya kibondo Bw. Seif Salum amesema kiwango cha bei ya ushuru kilichopangwa hakizidi aslimia tano ya bei za mazao, na kuwataka wafanyabiashara kuzingatia kanuni na sheria zinazokuwa zimepangwa na halmashauri kwa kuzingatia msimu wa upatikanaji wa bidhaa za kilimo.

“Cha msingi ni kuzingatia tu mana mabadiriko yaliyofanyika si kwa lengo la kuwakomoa au kujinufaisha bali kwa lengo la kuinufaisha halmashauri pamoja kuangalia ugumu wa upatikanaji wa bidhaa husika” amesema.