Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Mar 22, 2018

AJARI YAUA WATU 7 KIGOMA

WATU saba wamefariki dunia baada ya gari  aina ya scania lenye namba za usajili T. 741 AAB baada ya kupinduka katika eneo la mkongoro likitokea kalinzi kuelekea kigoma mjini.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa kigoma Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa ajari hiyo na kusema kuwa chanzo ni uzembe wa dereva wa gari hilo.

 Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa Maweni Dkt Fadhiri Kibaya majeruhi ni Michael Richard na waliofariki Katika ajari hiyo ni
Deodata Komba, Slimu Hamis, Ramadhani Said,
Elia Katabi,
Nashoni Bilonkwa, Omary Mohamed na  Eliakim Samson.