Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jul 15, 2015

MASHABIKI LIVERPOOL WAMKARIBISHA MARCO REUS BAADA YA STERLING KUONDOKA



MASHABIKI wa klabu ya Liverpool wameiandikia barua Club hiyo na kumtaka Ian Ayre na mmi;liki wa klabu hiyo John W Henry kumsajiri kiungo mshambuliaji wa Borusia Dotmund Marco Reus kutokana na mauzo ya Raheem Sterling.

Kutokana na Muzo ya Sterling aliyetimkia Man City kwa dau la  Paun mil. 49, mashabiki hao wameona ni muda muafaka kwa klabu hiyo kumsajiri Reus ambaye wanatumaini ataziba pengo la Sterling kulingana na kiwango cha Mjerumani huyo.

Kwa upande wa Benteke ambaye anatakiwa kwa udi na uvumba na Liverpool, inasemekana dili hilo limeiva kwa mujibu wa Gazeti la Bergian ITK lililoibua taarifa za Origi kuja ‪#‎LFC na pia kuachwa kwa mkopo katika klabu ya Lile.

Muandishi Daniel Vander Lamp amedadavua kua dili iyo ina thamani ya €42m ambayo ni sawa na£29-30m jumlisha Rickie  Lambert.

Mashabiki HAWAJARIDHISHWA NA DILI IYO na  kuandika barua na kuanzisha "petition" ya kusaini wakihitaji mashabiki 200,000 kwa support ili Marco Reus atue Anfield.