Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jul 14, 2015

NYARA ZA SERIKALI ZAKAMATWA KIGOMA



JESHI la Polisi mkoani Kigoma limefanikiwa kukamata nyara za serikali zenye thamani ya Tsh. 37,625,000/=, kwenye maeneo ya Hifadhi ya Gombe kijiji cha Mgambazi wilaya ya Uvinza mkoani hapa.

Akizungumza na waandhishi wa habari hapo jana, Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, SACP Ferdinand Mtui, alisema kuwa, tukio hilo lilitokea Julai 13 majira ya saa 7: 00 mchana wakati Askari Polisi wakiwa kwenye msako kwa kushirikiana na Askali wa Hifadhi ya Gombe.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoa SACP Ferdinand Mtui

Kamanda Mtui alisema kuwa, Nyara hizo zilikamatwa nyumbani kwa Jackson Evarist (44) mkazi wa Mgambazi baada ya Polisi kufanya upekuzi nyumbani kwake kufuatia taarifa za Kiintelijensia kuhusu umilikaji wa nyara hizo kinyume cha sheria.

“Nyara zilizopatikana nyumbani kwa Jackson  ni pamoja na meno sita ya tembo yenye uzito wa kg 28 na thamani ya Tsh. 30,100,000/=, ngozi na fuvu moja la chui vyenye thamani ya  Tsh.7,525,000/= .

“Nyara  zote zilikuwa zimehifadhiwa katika mfuko wa sandarusi uliokuwa ndani ya chumba cha kulala mtuhumiwa” alisema  Kamanda Mtui.

Aidha Kamanda Mtui alisema kuwa, Upekuzi huo ulifanyika chini ya uangalizi wa Viongozi wa serikali ya Kijiji na Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Sambamba na kuwashukuru wananchi kwa taarifa walizotoa zilizopelekea kukamatwa kwa nyara hizo, Kamanda Mtui aliwataka wananchi mkoani hapa kutokuchoka kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kufichua  vitendo vya uharifu na waharifu.

Mwisho.