Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jul 16, 2015

UCHAFU WAWATESA WANANCHI KIGOMA



WAKAZI  wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wameiulalamikia uongozi wa Halmashauri kwa kushindwa kupambana na hari ya uchafu inayoikabili Manispaa hiyo kutokana na kuenea kwa uchafu katika maeneo ya watu.

Katika Manispaa ya Kigoma-Ujiji suala la usafi linaonekana kushindikana kutokana na uchafu unaozalishwa kila siku kutokusanywa na kupelekwa sehemu husika kwa muda muafaka na kusababisha uchafu kuzagaa hovyo licha ya wananchi kulalamikia suala hilo kila siku.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti, wakazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji walitoa malalamiko yao kuhusu hali ya uchafu katika manispaa hiyo.
Dampo la uchafu lililoko maeneo ya Mwanga Center ambalo ni moja ya dampo linalolalamikiwa kutokutolewa kwa uchafu.

Festo Yothamu ambaye ni mfanyabiashara wa vyuma chakavu eneo la Mwanga Centre alisema kuwa,  wanapata kero ya harufu mbaya pia muonekano wa uchafu  kutokana na dampo la uchafu lililoko maeneo yao ambalo hujaa kwa muda mrefu bila kuondolewa.

Alisema kuwa, dampo hilo linaathiri ya kutokuzolewa uchafu kwa muda muafaka kama yalivyo madampo ya maeneo mengine nakusababisha uchafu kuingia mpaka barabarani na kusogea karibia na maeneo ya kazi za watu huku harufu mbaya ikiendelea kuwa kero kwa watu kila siku.

Yotham aliongeza kuwa,  kuwa hari hii ya uchafu inaweza kupelekea mlipuko wa magonjwa hivyo serikali ambao ndio wana dhamana ya kuangalia usafi wa Manispaa waangalie ni wapi wanakosea ili kurekebisha tatizo hili.
Dampo la uchafu lililoko maeneo ya Mwanga Center ambalo ni moja ya dampo linalolalamikiwa kutokutolewa kwa uchafu.

Aidha Aisha Issa ambaye ni Mama Ntilie eneo la Mwanga Centre alisema kuwa dampo lililopo maeneo hayo limekuwa kero kubwa kwa biashara yake hasa kipindi harufu inapokuwa kali husababisha wateja kutokula chakula

Alisema kuwa wanajitahidi kutoa ushirikiano kwa serikali za mitaa ambazo zinasimamia zoezi la kukusanya uchafu kwenye makazi ya watu kwa kuchangia shilingi 1000/= ila bado serikali haijari kuondoa uchafu unaokusanywa katika dampo hilo.

“Hakuna mtu anayependa kula chakula sehemu nambayo inaharufu mbaya, sasa hapo ndio sisi wauza chakula tunakosa wateja kabisa’ alisema Issa.


Nae Abdara Kimenya ambaye ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Kisangani, alizungumzia zoezi la uzoaji wa taka majumbania kuwa zoezi hilo linaonekana kukwama kutokana na  changamoto ya kutokuwepo  kwa vitendea kazi kama matololi na mapipa ya kuhifadhia taka kabla hazijachukuliwa..

“Gari zinatakiwa kuwa Zaidi ya mbili pia serikali inatakiwa kugawa katika mitaa mapipa ya kuhifadhi uchafu kabla haujakusanywa, hata kama pipa moja likitumika kwa nyumba hata 10 ili kukomesha uchafu kuzagaa” alisema Kimenya.

Kwa upande wake Afisa Afya wa Manispaa ya Kigoma-Ujiji Leonida Mbwiliza, alisema kuwa suala la uchafu katika Manispaa lipo ila jitihada zinafanyika ili kupambana na suala la uchafu ambapo serikali za mitaa zinaendesha zoezi la kukusanya taka majumbani na kuzipeleka kwenye madampo.

Alisema kuwa changamoto zinazochangia kuwepo kwa uchafu ni kukosa vitendea kazi kutokana na Manispaa kuwa na gari mbili mabazo bado hazitoshi pia Mitaani vifaa vinahitajika ili kuwawezesha wakusanyaji wa uchafu majumbani kufanya kazi vizuri na kwa muda muafaka.

“Gari zilizopo kwanza ni za kizamani pia ni madogo, Gari moja linabeba tani tatu hivyo huzoa takataka kidogo wakati taka zinazozaliishwa ni nyingi, ukweli magari haya yameshachoka leo zima kesho bovu sasa huwezi kutegemea magari hayo” alisema Mbwiliza.