Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Dec 1, 2015

MAJAMBAZI WAWILI WAUWAWA KIGOMA



WATU wawili wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa baada ya kushambuliana kwa risasi na askari polisi waliokuwa kwenye dolia katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

Akizungumza na Waandishi wa habari hii leo, Kamanda wa polisi mkoani Kigoma, SACP Fednandi Mtui alisema kuwa, tukio hilo lilitokea November 27 majira ya saa tisa alasiri ambapo watu hao hawajafahamika hadi sasa huku miili yao ikiwa imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika hospital ya wilaya ya Kasulu mkoani hapa.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SACP Ferdinand Mtui, akionyesha siraha aina ya SMG waliyokuwa nayo majambazi waliouwawa.

Alisema kuwa, awali watu hao walipola vitu mbalimbali na kukimbia navyo, baada ya raia wema kutoa taarifa, polisi walifika na kufanya  msako hatimaye  kuwakurupusha majambazi hao waliokuwa wamejificha kwenye vichaka.

“Baada ya kuwakurupusha  walianza  kurushiana risasi ambapo Polisi waliwajeruhi na baada ya kuwakamata waliwapekuwa na kufanikiwa kuwakuta na siraha moja aina ya SMG iliyokatwa mtutu na kitako,  pia walikuwa na magazine tatu huku mbili zilikuwa na risasi 60 na risasi zingine 33 zikiwa kwenye mfuko wa naironi” alisema Kamanda Mtui.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SACP Ferdinand Mtui, akionyesha magazine ambazo ndani zina jumla ya risasi 59.
Aidha Kamanda Mtui alisema kuwa, vitu vilivyoibwa na watu wale kutoka kwa wakimbizi  wa kambi ya Nyarugusu ni pamoja na simu mbili, Vocha 45 za mitandao miwili tofauti pamoja na nguo mbalimbali.

Aliongeza kuwa, kutokana na majeraha waliyokuwa nayo majambazi wale ilibidi wapelekwe hospitali kwaajiri ya matibabu lakini kabla ya kufikishwa walifariki hivyo  miili hiyo kuhifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti.

Hata hivyo  Kamanda Mtui aliwaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo na kutoa taarifa pale wanapoona watu wanaowatilia mashaka ili kudhibiti matukio kabla ya kutokea.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SACP Ferdinand Mtui, akionyesha Vocha  zilizoibwa kwa wakimbizi wa kambi ya Nyarugusu.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SACP Ferdinand Mtui, akionyesha Vocha  zilizoibwa kwa wakimbizi wa kambi ya Nyarugusu.
Risasi zilizokutwa ndani ya mfuko.