Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Dec 27, 2015

GARI LA RPC KIGOMA LAMGONGA BODABODA NA KUFA PAPO HAPO



MTU mmoja ajulikanaye kwa jina la Gerevasi Kassiano(25) ambaye ni dreva bodaboda mkazi wa Burega amefariki dunia baada ya kugongwa na gari linalotumiwa na Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Ferdinand Mtui.

Akizungumzia tukio hilo Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Masud Kalembe ambaye ni shuhuda wa tukio hilo alisema kuwa, tukio hilo lilitokea Desemba 26 mwaka huu majira ya saa 8.30 mchana eneo la Lubengera katika Manispaa ya kigoma Ujiji ambapo  gari aina ya Landcruser yenye vioo  vyeusi (tinted) linalotumiwa na RPC lilimgonga kijana huyo na kufa papo hapo.

Alisema kuwa, gari hilo lilikuwa likitokea barabara ya Kigoma Ujiji kwenda kigoma mjini, na baada ya dreva wa gari hilo kuyapita kwa pamoja magari mawili ya abiria (Hiace) yaliyokuwa yakifuatana akajikuta  akigongana uso kwa uso na dereva wa bodaboda na kufa hapohapo.

“Maiti ilitolewa chini   ya gari la RPC, na kitendo hicho kilipelekea baadhi ya madereva wa bodaboda kituo cha Lubengera kufunga njia wakitaka haki  itendeke ndipo askari waliovaa kiraia waliokuwa katika gari la defender  walipiga bomu moja la machozi ili kuwatawanya raia, hapo hapo vijana wawili walikamatwa na kutupwa mahabusu huku pikipiki tatu zikishikiliwa na jeshi hilo.

“Ili kuinusuru serikali ya awamu ya tano isionekane ya kufumbia macho matukio yoyote yale, sikuwa na budi kuwafuatilia vijana hao hadi wakatolewa kwa ushirikiano wa Mkuu wa wilaya Saveli Mwangasame, ila nachojiuliza kwa nini baadhi ya askari wanajawa na vibuli vya magwanda tu wakati Watanzania wote tuha haki sawa” alisema Kalembe.

Adha baadhi ya waendesha bodaboda kituo cha Maweni na Lubengela wakiomba hifadhi ya majina kwa usalama wao katika shughuli zao, kwa nyakati tofauti walikiri kutokea kwa tukio lilomuua mwenzao.

Nae Mganga Mfawidhi hospitali ya rufaa Maweni, Fadhili Kibaya, alikiri kupokea  maiti ya kijana aliyegongwa na gari mida ya saa 9:00 alasiri na maiti kuhifadhiwa chumba cha mochwari kwa ajili ya taratibu zingine.

Kwa upande wa Kamanda wa Polisi mkoani  Kigoma, SACP  Fernand Mtui, alipohojiwa kwa njia ya simu juu ya tuko hilohilo alijibu kuwa “Ni kweli ila ajari hiyo ni kama ajari zingine, ndugu wakitaka maelezo kamili waje kituoni watapewa namna ilivyokuwa”.

Hata hivyo leo hii Desemba 27 asubuhi ya saa 4 zilionekana gari mbili eneo la tukio na kuona shughuli ya upimaji wa ajali ikifanyika chini ya ulinzi mkali, hali inayowashangaza raia kwa jeshi hilo kushindwa kuwajibika pale wanapokosea wao.