Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Dec 13, 2015

TFDA YAKAMATA TANI TATU ZA BIDHAA FEKI KIGOMA


MAMLAKA ya chakula, dawa na vipodozi nchini (TFDA) imekamata na kuteketeza kwa moto tani tatu za bidhaa mbalimbali mkoani Kigoma ikiwemo vipodozi, dawa za binaadam na mifugo na vyakula vyenye thamani ya shilingili milioni nane na nusu ambavyo vimepigwa mafuruku na vingine muda wake wa kuuzwa umeisha.

Zoezi la uchomaji moto wa bidhaa  hizo ulifanyika  katika dampo la Lusimbi  Manispaa ya Kigoma –Ujiji mkoani hapa kwa kusimamiwa na Meneja wa TFDA kanda ya Magharibi, Dk. Edger Mahundi.


Akizungumzia tukio  hilo wakati wa kuteketeza bidhaa hizo, Dk. Mahundi alisema kuwa, bidhaa hizo walizikamata maeneo mbalimbali mkoani hapa kutokana na msako waliofanya kwa kushitukiza na kufanikiwa kukamata bidhaa mbalimbali zilizopigwa marufuku na zile zilizoisha muda wake.

Alisema kuwa, bidhaa hizo walizikamata kwa kushirikiana na maofisa kutoka kanda hiyo ya magharibi  pamoja na wenzao waliopo mkoani hapa na aliwataka wamiliki wa maduka kufuata sheria za (TFDA) ambapo bidhaa zikiisha muda wake wawe wanaziondoa wenyewe dukani na kwenda kuziteketeza kwa moto.


“Zoezi hilo la msako wa kusaka bidhaa feki na zisizofaa kwa watumiaji niendelevu na litakuwa la kushtukiza kwa Mkoa wa Kigoma hivyo wafanyabiashara ni vyema muwe waaminifu” alisema Dk. Mahundi.

Naye Ofisa Afya wa bandari ya mkoa wa Kigoma na Mkaguzi wa mipaka, Theodory Rutahindurwa, alisema kuwa, wafanyabiashara wasiowaaminifu wamekuwa wakipitisha  bidhaa nyingi ambazo ni feki kwa njia ambazo siyo za halali jambo ambalo huhatarisha maisha ya watumiaji.

“Wito wangu kwa wafanyabiashara ni  kutii sheria zilizowekwa na kwa wafanyabiashara watakaobainika na kukutwa na makosa hayo tena watafungiwa leseni zao sambamba na kufikishwa mahakamani” alisema Rutahindurwa.