Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Dec 30, 2015

WAZIRI MKUU AWATAKA WAKIMBIZI KUTOKUJA NA SIRAHA NCHINI



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa, amewataka wakimbizi wanaokuja nchini ili kuomba hifadhi kuacha kubeba siraha nakujanazo nchini kwani kwa kufanya hivyo kunachochea vitendo vya kiharifu.

Akizungumza na wakimbizi wa kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma hapo jana, Waziri Mkuu alisema kuwa, kumekuwa na vitendo vingi vya ujambazi wa kutumia sirahamkoani hapa ambapo utafiti unaonyesha matukio mengi hufanywa na raia wa kigeni.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, akizungumza na wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu iliyoko Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma.
Alisema kuwa, kwakuwa wakimbizi wote wako nchini ili kuokoa maisha yao kutokana na machafuko nchini kwao hawana budi kufuata sheria na taratibu za nchi ya Tanzania ili waipate ile amani waliyoifuata.

“Sawa tumewapokea na kuwapa hifadhi ila jambo la msingi ambalo hamtakiwi kulifanya ni kuja na siraha ya aina yoyote kambini, kama mtu anataka kuja nchi na ana siraha ni vyema aiache huko badala ya kuja nayo na kumletea madhara” alisema Waziri Majaliwa.

Aidha Waziri Majaliwa, aliwataka wakimbizi wote walio na siraha wazisalimishe ili kambi ziwe na usalama badala ya kusubiri mtu kukamatwa na siraha jambo ambalo litamuweka matatani.
Baadhi ya wakimbizi kutoka Burundi na Congo waishio katika kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu wakimsikiliza Waziri Mkuu Kassimi Majaliwa (hayupo pichani) wakati akiwahutubia.
“Kama kuna mtu umeficha siraha mahari popote ni vyema ukatumia busara kwa kwenda kuichukua na kuikabizi kwa Jeshi la Polisi badala ya kusubiri mpaka tukukamate, na tukikukamata lazima uchukuliwe hatua mana hatutaki kuhifadhi majambazi bali tunahifadhi raia wema.

 “Suala la usalama ni la muhimu kwa kila mkimbizi pia ni muhimu kwa majirani ambao ni watanzania sambamba na watoa huduma kambini humo, hivyo ni vyema kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake ili siku mkirudi nchini kwanu mrudi mkiwa salama” alisisitiza Waziri Majaliwa.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majariwa, akiangalia ngoma za jadi zilizokuwa zikichezwa na Wakimbizi raia wa Burundi katika kambi ya Nyarugusu.
Akitoa maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu, Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu, Sospeter Boyo, alisema kuwa, kambi hivyo ilifunguliwa Novemba 1996 kwa lengo la kuhifadhi wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kocngo waliokuwa wakikimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini kwao.

Alisema kuwa, kambi hiyo yenye ukubwa wa kilometa za mraba 28, ina uwezo wa kuhifadhi wakimbizi 50,000 lakini kwasasa ina wakimbizi 151,032 ambao ni mara tatu ya zaidi ya uwezo harisi wa kambi hiyo.

Boyo aliongeza kuwa, tangu Aprili mwaka huu, idadi ya wakimbizi iliongezeka hadi kufikia 151,032 ambapo miongoni mwao ni Wakongo 61,313, Warundi 89,619, Wanyarwanda 75, Waganda 12, Wasudan Kusini wane, Wakenya wane, Msomali mmoja, Mzimbabwe mmoja na Mwaivory Cost mmoja.