Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Jul 17, 2015

MOTO WATEKETEZA OFISI ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO



AJARI ya moto imetokea mkoani Kigoma na kuteketeza Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo huku chanzo chake kikiwa bado hakijajulikana.

Wakizungumza na Tanzania Daima mashuhuda wa tukio hilo ambao ni walinzi wa ofisi hizo, Ndaimisi Gwakila alisema kuwa, tukio hilo lilitokea mida ya saa 7 kasoro usiku wakati wakikagua usalama wa ofisi hizo.

Alisema kuwa, wakati wakiendelea na ukaguzi wakaona moto unawaka  kwenye paa ya jingo hilo ikabidi waombe msaada kwa Polisi waliokuwa wakilinda Benk ya CRDB jirani na ofisi hizo ndio wakafanya taratibu za kuzima moto ule.


“Kwa kushirikiana na Polisi wale ilibidi tutoe taarifa Kituo cha Polisi, Polisi walikuja na ila maji yalikuwa ni tatizo.

“Wananchi wa maeneo haya na viongozi waliopata taarifa walijitahidi kushirikiana kuzima moto lakini ilishindikana ikabidi waanze kubomoa sehemu ambazo moto ulikuwa hauwaki sana na kutoa vitu” aliserma Gwakila.

Nae Kamanda wa Polisi Wilayani humo, Marco Joshua alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa, kilichofanya washindwe kuzima moto ule baada ya kupata taarifa ni kutokana na kutokuwepo kwa kikosi cha zimamoto kwani kama kikosi hicho kingekuwepo ingekuwa rahisi kuzima moto ule.

“Kinachofanya kikosi hicho kisiwepo ni kutokana na tangu nishati ya umeme kuingia wilayani hapo hakujawahi kutokea janga kama hilo ila kwasasa inabidi serikali iangalie suala ya kuweka kikosi cha zimo Kibondo” alisema Joshua

Kamanda Joshua aliongeza kuwa, chanzo cha moto huo bado hakijajulikana ila wanaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha moto huo.

Kwa upende wake Mkurugenzi wa Maendelea ya Halmashauri hiyo, Juda Fabrious, alisema kuwa moto hupo uliteketeza ofisi za masijara ya wazi na ya siri, ofisi ya utumisi pamoja na Ofisi yake Mkurugenzi.

“Vitu vyote vilivyokuwemo ndani ya ofisi hizo viliteketea hivyo tunasubiri watu wa kufanya tathimini waje ili kujua gharama ya vitu vilivyoteketea” alisema Fabrious.