Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Dec 24, 2015

MCHUNGAJI WA FPCT AFARIKI DUNIA KATIKA AJARI YA GARI KUUNGUA MOTO KIGOMA



Mchungaji wa Kanisa la Free Pentecoste  Church of  Tanzania (FPCT) Songambele Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma Peter Sungura amefariki dunia katika ajari ya gari liloungua moto na kuua watu saba na kujeruhi wengine kumi.

Akizungumza na blog hii, Mchungaji wa Kanisa la FPCT Bigabiro mkoani hapa, David Nkone, amesema, mchungaji aliyefariki ni Peter Sungura ambaye alikuwa akisimamia Parishi ya Songambele kwa upande wa kanisa hilo.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SACP Ferdinand Mtui, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu tukio la ajari ya gari kuungua moto na kuua watu saba na kumi kujeruhiwa.
Amesema, taarifa za kifo hicho alizipata baada ya kupigiwa simu na mchungaji mwenzake ambapo alifika hospitali ya Mkoa ya Maweni na alipoingia chumba cha kuhifadhia maiti alithibitisha kuwa Mchungaji Sungura ni moja ya watu waliofariki katika ajari hiyo.

“Maelezo ya Madaktari wanasema katika majeruhi walifikishwa hospitalini hapo na mchungaji Sungura alikuwemo lakini ilipofika saa 6 usiku alifariki dunia kutokana na kuungua vibaya” amesema Mch. Nkone.

Aidha Mch. Nkone amesema, awali kabla ya tukio hilo Mchungaji huyo alikuwepo katika ofisi za makao makuu ya jimbo (Bigabiro) na baada ya kumaliza masuala ya kikazi alirudi Kigoma mjini kwa masuala yake binafsi.

“Baada ya kumaliza shughuri zake huko Mjini ndipo akaanza safari ya kurudi katika kituo chake cha kazi huko Songambele ambapo ndipo ajari ilimkutia katika gari alilopanda na kusababisha umauti wake” aliongeza Mch. Nkone

 Hata hivyo Mch. Nkone amesema kuwa taratibu za mazishi zimeshaanza na marehemu atazikwa katika kijiji cha Songambele ambapo kuna familia yake na maziishi hayo yatafanyika siku ya kesho Desemba 23 mara baada ya mwili kuwasili kijijini kule.

Kwa upande wake Mchungaji wa FPCT Mwanga katika Manispaa ya  Kigoma-Ujiji, Willison Gwimo, amesema kuwa taarifa za kifo cha Sungura amezipata mara baada ya kufika hospitalini kwa lengo la kwenda kuona wagonjwa.

“Baada ya kufika Hospitali nilikutana na kundi la watu ndipo wakanipa taarifa za ajari na kuniambia kuwa moja ya watu waliofariki na mchungaji wa kanisa letu yumo, ikabidi nifike chumba cha kuhifadhia maiti, na kweli nilikuta mwili wa mchungaji Peter Sungura hivyo nikaamua kuwa taarifu wachungaji wenzangu” amesema Mch. Gwimo.

Nae Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, SACP Ferdinand Mtui, amethibitisha kutokea kwa ajari hiyo iliyohusisha gari aina ya Toyota Hiace lenye namba T.700 kupinduka na kuwaka moto katika Kijiji cha Mwakizega Wilayani Uvinza  ikiwa ni majira ya saa 11 jioni ambapo gari hilo lilikuwa  likitokea Kigoma mjini kuelekea Kijiji cha Subankara.

Alisema kuwa, katika ajari hiyo watu saba wamefariki dunia na wengine kumi kujeruhiwa na chanzo cha ajari hiyo ni baada ya dreva kujaribu kuwakwepa watembea kwa mguu waliokuwa wakikatiza barabarani ambapo gari lilielekea upande mwingine na kugonga ukingo wa barabara na kuangua kisha kuwaka moto.