Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

Dec 24, 2015

WAHAMIAJI HARAMU 75 WAKAMATWA KIGOMA



Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limewakamata wahamiaji haramu 75 wakijihusisha na shughuri za kilimo mara baada ya kufanya msako katika Wilaya za Kasulu, Uvinza na Kigoma mjini.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, SACP Ferdinand Mtui, amesema kuwa wahamiaji hao walikamatwa wakiwa mashambani wakiendelea na shughuri za kilimo.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma SACP Ferdinand Mtui, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu tukio la kukamatwa kwa wahamiaji haramu.
Amesema, mbali na kuwakamata wahamiaji hao Polisi waliwakamata pia wahusika wa mashamba hayo ambao ni Watanzania kutokana na kuvunja sheria kwa kuwatumikisha raia wa kigeni bila kufuata sheria.

“Wahamaiji hao watafikishwa mahakamani ili kujibu mashitaka yao ya kuingia nchini kinyume na sheria wakati wamiliki wa mashamba watatakiwa kujibu mashitaka ya kuwatumikisha wahamiaji haramu kinyume na sheria” alisema Kamanda Mtui.

Kwa upande wake Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Kigoma, Maurice Kitinusa, amesem, taarifa za msako wa wahamiaji haramu anazo ila bado hajapata idadi kamili ya wahamiaji waliokamatwa.

“Nilipigiwa simu na Afisa uhamiaji wa Wilaya ya Kasulu kuhusu msako huo na mafanikio yake ila kwakuwa idadi kamili sijaipata basi tusubiri mpaka baada ya sikukuu ndio tutatoa idadi kamili kwa mkoa mzima” alisema Kitinusa