Kigoma Online News

FURNITURE

KALIHAMWE STATIONARY

KALIHAMWE STATIONARY

May 18, 2016

WANANCHI KIGOMA WAPONGEZA MRADI WA TUUNGANE


Wakazi wa mkoa wa Kigoma waishio mwambao mwa ziwa Tanganyika wameupongeza mradi wa TUUNGANE kwa hatua uliyofikia katika kusimamia utunzaji wa mazingira ya mlima wa Hifadhi ya Mahale pamoja na ziwa Tanganyika yaliyokuwa yakiharibiwa na wakazi hao kutokana na ukosefu wa elimu.

Mradi huo wa TUUNGANE unaotekelezwa na shirika la la Pathfinder international na the nature conservancy unaolenga utunzaji wa mazingira na afya umefanikiwa kwa zaidi ya asilimia 90 mkoani Kigoma katika milima ya hifadhi ya mahale na Ziwa Tanganyika kutokana mbinu mbalimbali zilizotumika katika utekelezaji wake.

Wakizungumza na blog hii mkoani humo, Lukasi Kanoni na Lusia Mathias ambao ni wakazi wa Kalya walisema kuwa, mradi huo umefanikiwa kutokana na kuwa njia iliyotumika katika utekelezaji wa wake ilikua shirikishi ambapo mazoezi ya utunzaji mazingira yalifanyika kwa vitendo.

“tuwapongeze wasimamizi wa mradi kwa hatua hii waliyofikia, tulifundishwa kwa vitendo kama namna maji ya ziwa yanavyochafuliwa na vinyesi kutoka vichakani kwa wakazi wasio na vyoo, lakini tulifundishwa kutochoma msitu katika maeneo yetu” alisema Mathiasi

Meneja mradi Petro Masolwa alisema, mradi unatekelezwa wilayani Uvinza mkoani Kigoma  ambapo lengo ni kutunza mfumo wa Ikolojia ya Milima ya Mahale na mazinira ya ziwa Tanganyika na kusema kuwa mradi ulianza 2011 ukienda sambamba na masuala ya utengamano kati ya watu, afya na mazingira yanayowazunguka.
  
Masolwa alisema kulinda ardhi na misitu, maji na samaki wa ziwa Tanganyika, afya ya uzazi (nyota ya kijani), pamoja na afya ya msingi ni moja ya malengo ya mradi  ambapo mpaka sasa malengo hayo yameweza kutimia kwa asilimia 90 na mpaka sasa  mikakati iliyowekwa na mradi ni kuboresha utawala bora ngazi ya vijiji, usimamizi wa rasilimali ardhi na misitu, uvuvi endelevu, pamoja na mawasiliano katika maeneo hayo.

“tumefanya hivyo ili kupata urahisi wa kazi ya utunzaji utekelezaji wa mradi, wakazi wa vijiji hivyo 24 walikua wakikabiliwa na changamoto za huduma za kijamii ambapo tumetatua changamoto hizo hivyo wakazi hao kutuunga mkono katika shughuli nzima” alisema Msolwa.

Afisa mawasiliano mradi Nelson Mmali alisema, mradi umetoa mafunzo kwa vingozi wa vijiji na askali lengo ikiwa ni kuwafanya watambue majumkumu yao ulinzi wa misitu na kwamba katika kutekeleza huduma za kijamii zahati za vijiji hivyo zimekarabatiwa, mafunzo kwa wahudumu wa afya yametolewa pamoja na kuweka miundo mbinu ya umeme wa jua.

Hata hivyo kutokana na vijiji hivyo kukikabiliwa na changamoto ya magonjwa ya mlipuko usafi umehamasishwa ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vyoo bora lengo ikiwa ni  kuzuia kujisaidia vichakani hali inayochangia uchafuzi wa maji ya Ziwa Tanganyika.

Iddi Ndabhona ambaye ni mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Kigoma alisema wananchi wa Vijiji vya Sibwesa, Buhingu, Kalya na Katumbi wametunga sheria ndogondogo zikiwa na lengo la kuboresha uhifadhi wa mazingira pamoja na kuongeza kipato cha wakazi hao.

Ndabhona aliupongeza mradi huo na kusema kuwa , kutokana na sheria hizo kufuata matakwa yote ya kisheria kikao cha baraza la madiwani kilidhia kutumika kwa sheria hizo ambazo zinahusisha uhifadhi wa mazingira na kudhibiti uvuvi haramu katika ziwa Tanganyika.